Ruka hadi kwenye maudhui makuu

ANTOINE GRIEZMANN: "NIMEKUWA NIKISUBIRI KUHAMIA ARSENAL"

Mfaransa huyo alikuwa akisubiri kwa hamu kutua Emirates, lakini mambo hayakwenda kama alivyotarajia na fursa ilipomjia tena alikataa na kuwapotezea
Mshambuliaji wa Atletico Madrid Antoine Griezmann amebainisha kuwa alikaribia kujiunga na Arsenal 2013, lakini alikasirika baada ya klabu hiyo kuacha kumfuatialia.

Griezmann ambaye, alikuwa akicheza Real Sociedad miaka minne iliyopita, alikuwa kivutio kwa Gunners baada ya wakala wa Mfaransa huyo, Eric Olhats, kuwa kwenye mawasiliano na Giles Grimandi wa Arsenal.

Uhamisho huo ulishindikana kukamilika, hata hivyo, Griezmann alijiunga na klabu yake ya sasa Atletico 2014, na mshambuliaji huyo ameeleza jinisi alivyoitosa Arsenal baada ya kuona klabu nyingine zinahitaji huduma yake.
"Nilisubiri, nikasubiri na kusubiri," Griezmann aliandika kwenye ukurasa wake mpya. "Kulipokuwa hamna habari, Eric alimpigia Grimandi, ambaye alisema kuwa bado meneja alikuwa akivutiwa na mimi na tukaendelea kusubiri.

"Hatimaye, saa chache kabla ya soko kufungwa, alitufahamisha kuwa Arsenal haiwezi kukamilisha usajili. Sipendi kuambiwa jambo alafu lisitokee.
"Kwa hiyo, Eric aliniambia baadaye kuwa klabu hiyo ya London ilikuwa ikitamani huduma yangu tena, nilimwambia 'chana nao, baada ya kutuangusha'".

Griezmann alifunga mara mbili timu yake iliposhinda 5-0 dhidi ya Levante wikiendi iliyopita, matokeo mazuri kufuatia ushindi mwingine wa Atletico wa 2-0 dhidi ya Roma.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Nitapindua dunia juu chini ili kubaki kama meneja wa Arsenal

Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake. Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal Kazi yake katika timu hiyo iliwekwa utatani wakati alipokataa kudhibitsha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror) Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)

Robert Lewandowski mfungaji bora Bundesliga 2017/2018

Robert Lewandowski amemaliza msimu wa 2017/18 wa Bundesliga akiwa mfungaji bora kwa mara ya 3 kwenye maisha yake ya soka. : • 30 games • 29 goals

Je Barcelona wataweza kuvunja rekodi hizi?

Hadi sasa miamba  ya Catalunya Fc Barcelona haijapoteza mchezo hata mmoja katika ligi kuu nchini Hispania na wanaonekana wanaweza kuweka rekodi ya kuwa timu pekee kumaliza La Liga bila kupoteza, lakini je na haya yafuatayo wataweza? Magoli 121, Jose Mourinho msimu wa 2011/2012 alimaliza La Liga akiwa na mabao 121, hadi sasa Barcelona wana mabao 70 na itawabidi kufunga mabao 51 katika mechi zao 11 zilizobaki ili kuifikia rekodi ya Mourinho. Zamora award, hii ni tuzo ya kipa aliyefungwa mabao machache, Francisco Liano mlinda lango wa zamani wa klabu ya Sporting Gijon anashikilia rekodi ya kufungwa mabao machache zaidi La Liga, mabao 18 (1993/1994). Hadi sasa mlinda lango wa Atletico Madrid Jan Oblak ameruhusu mabao 12 katika lango lake huku golikipa wa Barcelona Marc Andre Stegen akiwa ameruhusu mabao 13 hadi sasa, na anasubiriwa kati ya hawa nani atavunja rekodi ya Liano. Real Sociedad record, Barcelona hawajapoteza katika michezo 32 ya La Liga na wamevunja rekodi ya Pep G...