Yanga imechoshwa na visa na vituko vya mshambuliaji wake Mzimbabwe Donald Ngoma na sasa inapanga namna ya kumwajibisha Klabu Yanga imepanga kumuwajibisha mshambuliaji wake raia wa Zambabwe Donald Ngoma, kwa kosa la kwenda kwao bila ruhusu ya klabu hiyo ambayo anaitumikia kwa msimu wa tatu sasa. Chanzo cha bari kutoka ndani ya klabu hiyo kimeiambia Goal , kuwa uongozi wa juu upo katika mjadala wakijadili namna ya kumwadhibu mchezaji huyo ambaye hajaichezea timu yao kwa miezi miwili baada ya kutimkia kwao Zimbabwe bila ruhusa ya klabu. "Tupo kwenye kikao cha kumjadili Ngoma, amekuja jana kutoka kwao Zimbabwe tunachotaka ni kutuambia nani alimpa ruhusa ya kwenda kwao na kingine tunataka kujua kama anataka kucheza Yanga au kuondoka maana tunashindwa kumuelewa kwa yale anayotufanyia," imesema taarifa hiyo. Chanzo hicho kimedai pamoja na majeruhi aliyokuwa nayo mchezaji huyo lakini alipaswa kubaki nchini kwa ajili ya kufanyiwa matibabu kama ilivyo kwa wenzake wawili Amissi Tamb...