Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari, 2018

Lucas Moura kuelekea Tottenham.

Tottenham ina matumaini ya kunasa saini mchezaji wa Paris St-Germain Lucas Moura kwa ada zaidi ya £ 20m. Mchezaji wa kimataifa wa Brazil, 25, amekutana na meneja wa Spurs Mauricio Pochettino na mwenyekiti Daniel Levy na anataka kukamilisha hatua hiyo. Lucas alijiunga na PSG kwa £ 33.5m kutoka Sao Paulo mwaka 2013 lakini ameonekana mara sita tu  msimu huu na ameambiwa anaweza kupata klabu mpya. Ameshinda vikombe 13 vya ndani wakati akiwa nchini Ufaransa, ikiwa ni pamoja na vikombe vya ligi vinne.

De Gea: "Nina furaha Manchester United"

David de Gea amejitangaza mwenyewe kuwa "mwenye furaha sana" huko Manchester United huku kukiwa na fununu zinazoendelea kuhusu suala la yeye kujiunga na vigogo wa La Liga Real Madrid. "Unapofikiri niko msimu wangu wa saba sasa, mimi nina furaha sana japo kuna jambo moja au mawili ambayo hayajakaa sawa lakini bado ninafuraha sana. Nilikuja hapa kama mtoto lakini sasa ni mwanaume ndani na nje ya ya uwanja. Nikitazama nyuma ni miaka mizuri ajabu" alisema Mhispania huyo.

Beki mwingine ghali kujiunga na Man City.

Athletic Bilbao imethibitisha kwamba Manchester City imewasilisha ada kwa ajili ya kuvunja mkataba  wa Mfaransa Aymeric Laporte, ikiaminika kuwa wenye thamani ya € 65m. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 atajiunga na kikosi cha Pep Guardiola mwishoni mwa wiki hii.

Mourinho: "Siwezi kumzuia Ibrahimovic kuondoka"

Jose Mourinho amesema hawezi kumzuia Zlatan Ibrahimovic endapo atataka kuondoka Manchester United ikiwa mshambuliaji wa Kiswiden ataaonyesha hamu ya kuondoka. Pamoja na kuwepo kwa fununu kuwa mchezaji huyo anaweza kwenda La Galaxy, Mourinho amesema "Hakuniambia kitu kuhusu hilo mara ya kwanza nilivyosoma au kusikia kuhusu hilo kilichotokea kutoka kwa waandishi wa habari. Yeye hakuniambia kitu kamwe kuhusu hilo hivyo sijui . "    "Ni mwaka wa mwisho katika mkataba wa Zlatan Ibrahimovic . Ikiwa ni kweli  Zlatan anataka kwenda katika klabu nyingine katika nchi nyingine tuko hapa kusaidia na kuunda mazingira kwa ajili hiyo, sio kufanya maisha yake kuwa magumu."

Messi aweka rekodi nyingine dhidi ya Ronaldo.

Mkwaju wa faulo wa moja kwa moja kutoka kwa Lionel Messi dhidi ya Alaves siku ya Jumapili uliipa Barcelona ushindi wa 2-1, na pia ulimfanya mchezaji huyo wa Argentina kumzidi hasimu wake Cristiano Ronaldo kwa kufunga mikwaju mingi ya faulo. Mechi ya Jumapili ilikuwa ni hatua nyingine muhimu kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 ambaye alicheza mchezo wake wa 200 Camp Nou.

Luis Suarez na Messi waingoza Barcelona katika ushindi.

Usiku wa jana ulikuwa usiku wa kipekee kwa vijana wa Catalonia baada ya kupata ushindi wa kutokea nyuma dhidi Alavez na kushinda [2-1] Atletico Madrid ya walishinda 3-0 dhidi ya Las Palmas mapema Jumapili iliweka msimamo wa shinikizo kwa viongozi wa ligi na vijana wa Ernesto Valverde. Philippe Coutinho alianza tangu dakika ya kwa kabla ya kufanyiwa substitution na kuingia Paco Alcacer. Msimamo wa Alavez unabaki pointi mbili juu ya eneo la kushuka daraja na waliachwa kwenye taharuki walipataopoteza nafasi wakati Luis Suarez funga bao la kwanza dakika ya 72 na Messi kupigilia msumari wa pili na wa ushindi dakika ya 81. Kwa sasa Messi ndio kinara wa mabao katika ligi ya Uhispania, La Liga akiwa na mabao 20. Barcelona inabakia kileleni kwa pointi 11 dhidi ya vijana wa Diego Simeon, Atletico Madrid.

Aubameyang karibuni kujiunga Arsenal

Arsenal iko karibu na kunasa saini ya Pierre-Emerick Aubameyang kutoka Borussia Dortmund baada ya vilabu kukubaliana ada ya £ 60 milioni. Mchezaji huyo, ambaye alifunga mabao 31 ya ligi msimu uliopita, alisalia nje ya michezo miwili mfululizo ya Dortmund baada ya kukosa mkutano wa timu, na kocha mkuu Peter Stoger akimshtaki kuwa na kusubiri. Hata hivyo, Aubameyang alianza kucheza katika kikosi cha Dortmund dhidi Freiburg Jumamosi kukiwa na madai kutoka upande wa Bundesliga kuwa uhamisho ungeidhinishwa kama Arsenal ingefikia 'vigezo fulani'. Aubameyang atajiunga na mchezaji wa zamani wa Dortmund Henrikh Mkhitaryan huko Arsenal baada ya Muarmenia huyo kujiunga na klabu hiyo katika mkataba wa ubadilishaji ambao ulimpeleka Alexis Sanchez  Manchester United.

Madrid kufanya kufuru ya pesa EPL

Siku hizi kila mahali pesa ndio kila kitu, mwenye pesa anaweza kugeuza kila kitu ndani ya muda mfupi. Hivyo ndio unavyoweza kusema baada ya Florentino Perez kuamua kutangaza vita kubwa sokoni. Madrid wanaonekana kuyumba sana msimu huu na hakuna matumaini ya kombe lolote huku wapinzani wao Barcelona wakiwa katika msimu bora kuanzia uwanjani na hadi sokoni katika soko hili la usajili. Sasa Madrid wameamua kujiandaa kulipa kisasi katika manunuzi na kiasi cha £500m kimetengwa kwa ajili ya kufanya usajili wa nyota watatu wakubwa katika dirisha kubwa lijalo la usajili. £500m yote inaonekana kuelekezwa katika ligi kuu ha Uingereza EPL na kwanza wataanza na Manchester United ambapo watamwaga £100m kwa ajili ya kumsajili golikipa wa Manchester United David De Gea anayetajwa kuwa na thamani zaidi ya £75m. Madrid hawaishii hapo wanataka kuivamia tena Tottenham Hotspur na wanaamini kiasi cha £200m kinaweza kuwashawishi Tottenham kumuuza mchezaji wao bora kinara wa mabao...

Wenger na Pochettino wazozana

Kocha wa Arsenal wiki hii alitoa kauli ambayo imepokelewa vibaya na mashabiki wa Tottenham, wiki hii nzima mashabiki wa Tottenham mitandaoni wamekuwa wakimuandama Wenger. Wakati Wenger akiongea na waandishi wa habari alisema anashangazwa na jinsi waandishi wanavyoongea kuhusu Arsenal kukosa makombe na huku kuna vilabu kama Tottenham na Liverpool nao wako hivyo hivyo. Kocha wa Tottenham ameisikia kauli ya Wenger na kusema kwamba badala ya Wenger kujihusisha na kufuatilia mambo ya Tottenham inambidi awaze yeye kwanza kuhusu uwezo wao uwanjani. Pochettino amesisitiza kwamba anamuheshimu sana Arsene Wenger na asingependa kupoteza heshima yake kwa kumuongelea vibaya lakini kwa sasa anaona ni vyema azungumzie masuala ya Arsenal zaidi. Tottenham hawajachukua CL tangu mwaka 1984, hawajachukua EPL 1960/1961 na hawajachukua kombe la ligi tangu msimu wa 2007/2008 lakini Pochettino amesisitiza kwamba timu sio makombe tu ila hata wanavyokua ni jambo zuri.

Tetesi za soka Ulaya Ijumaa 26 Januari 2017

Baada ya Alexis Sanchez kuondoka Arsenal sasa klabu hiyo iko tayari kutuma ofa kwa PSG kwa ajili ya kumnunua Lucas Moura ambaye Arsene Wenger anamuona kama mtu sahihi wa kuvaa viatu vya Sanchez. Inadaiwa kwamba mshambuliaji wa klabu ya Arsenal Olivier Giroud anaweza kufanya usajili wa mshambuliaji wa Borussia Dortmund Pierre Aubameyang usitokee kwani hana mpango wa kwenda Dortmund. Kocha wa Real Madrid Zinedine Zidane amekiri kwamba kwa sasa kazi yake haiko mashakani sana lakini amekiri kwamba mechi yao na PSG inaweza kuamua hatma yake ndani ya klabu hiyo ya Real Madrid. Real Madrid wanataka kurudi tena kwa Manchester United kumuwinda mlinda lango wao David De Gea na taarifa zinasema kwamba tayari Madrid wameshamwambia wakala wa De Gea kuhusu nia yao hiyo. Pep Gurdiola anatajwa kuingia kwenye vita ya kumnasa Antoine Griezman toka Atletico Madrid na Manchester City wanataka kumtumia Kun Aguero aende Atletico na wao wamchukue Mfaransa huyo. Klabu ya As Roma imekanusha taarifa kwamba...

Sanchez tayari kujiunga na Man Utd, Mkhitaryan akubali kuhamia Arsenal

Mchezaji wa kiungo cha kati wa timu ya Manchester United Henrikh Mkhitaryan amekubali kujiunga na timu ya Arsenal, huku Alexis Sanchez akitarajiwa kuhama upande wa pili. Mkhitaryan, mwenye umri wa miaka 28,ambaye ni raia wa Armeniaatafanyia ukaguzi wa kimatibabu Leo Jumapili au kesho Jumatatu, huku Sanchez mwenye umri wa miaka 29 raia wa Chile atafanyiwa ukaguzi leo Juampili. Muda wa mkataba wa Mkhitaryan na kitita atakachopokea kama mashahara hakijulikani. Arsene Wenger awali alisema Sanchez atajiunga na United iwapo tu Mkhitaryan atahamia Arsenal. Sanchez alikosa ushindi wa Arsenal wa mabao 4-1 dhidi ya Crystal Palace Jumamosi kwasababu alikuwa anasafiri kwenda Manchester. "Huwezi kusafiri kwenda kaskazini na ucheze soka kwa wakati mmoja," alisema Wenger. Mkufunzi wa United Jose Mourinho, wakatihuo huo amesema mkataba wa kumsajili Sanchez unakaribia kukamilika kufuatia ushindi wa timu yake wa bao 1-0 dhidi Burnley Jumamosi. Timu hiyo ya Mashetano wekundu iliipiku Ars...

Tetesi za soka Ulaya Ijumaa 19 Januari 2017

Klabu ya Chelsea inatajwa kuingia rasmi katika vita ya kumnunua mshambuliaji wa As Roma Edin Dzeko ambapo Chelsea wanajipanga kutoa £50m kwa ajili ya mshambuliaji huyo pamoja na mlinzi wa kushoto wa Roma Emerson Palmieri. Juventus wanaonekana wamerudi katika klabu ya Arsenal na sasa wanataka kumchukua beki wao Hector Bellerin, Juventus wanatajwa kwamba wako tayari kutoa kiasi cha £40m kwa ajili ya kumnunua Bellerin. Klabu ya Manchester United inatajwa kuanza mazungumzo na golikipa wao David De Gea ili kujaribu kumuongezea mkataba, United wanataka kumpa De Gea mkataba mpya ili kumzuia asiende Real Madrid. Inadaiwa kwamba klabu ya Tottenham Hotspur imeingia katika vita na Manchester United kwa ajili ya kumsajili winga wa PSG Lucas Moura ambaye anatajwa kwamba siku zake kuitumikia PSG zimekaribia kuisha. Jean Michael Seri kiungo wa Ivory Coast anatajwa kuwaweka vitani Chelsea, PSG na Manchester City ambapo vilabu vyote hivyo vitatu vinatajwa kuhitaji huduma ya kiungo huyo wa ...

Zidane: "Hakuna Real Madrid bila Ronaldo"

Mkufunzi wa Real Madrid Zinedine Zidane anaamini kwamba mshambuliaji nyota Cristiano Ronaldo atasalia katika klabu hiyo na haoni sababu za yeye kuondoka katika klabu hiyo ya Uhispania. Mshambuliaji huyo wa Ureno amefunga magoli tisa katika mechi sita za vilabu bingwa lakini amefunga bao nne katika mechi 14 za la Liga msimu huu. Kulingana na ripoti , Ronaldo amekuwa na mgogoro wa kandarasi na klabu hiyo na amehusishwa na uhamisho wa kurudi Manchester United. Lakini Zidane alisema: Mimi hupendelea kusema kitu hicho hicho kwamba sioni Real Madrid bila Cristiano Ronaldo. Ronaldo mwenye umri wa miaka 32 yuko katika kandarasi hadi 2021 na alishinda taji lake la tano la Ballon d'Or mwezi uliopita, mbali na kufunga bao la pekee katika mechi ya fainali ya klabu bingwa duniani dhidi ya Gremio. Licha ya kuonyesha mchezo mzuri katika mechi za vilabu bingwa, wako katika nafasi ya nne katika ligi ya La liga baada ya kushindwa nyumbani na Vilareal siku ya Jumamosi. Tangu kujiunga na Real Ma...

Dortmund: "Wenger alitukosea heshima"

Mkufunzi wa Arsenal Arsene Wenger ''alitukosea heshima'' kwa kuzungumza hadharani kuhusu mchezaji Pierre-Emerick Aubameyang, amesema mkurugenzi wa michezo katika klabu ya Borussia Dortmund Michael Zorc. Arsenal ina hamu ya kumsajili mshambuliaji huyo wa Gabon kwa dau la £60m. Siku ya Alhamisi , Wenger alisema kuwa Aubameyang atafaa sana Arsenal , matamshi ambayo hayakuifurahisha klabu ya Dortmund. ''Tunahisi kwamba ni kukosa heshima kwa Wenger kuzungumzia kuhusu wachezaji wa klabu nyengine'', alisema Zorc. ''Hatujawasiliana na Arsenal''. ''Kwa sasa Arsene Wenger ana maswala mengi yanayompa changamoto ikiwemo mchezo wa wachezaji wake''. Aubameyang ameadhibiwa mara mbili kwa utovu wa nidhamu msimu huu. Alikosa mechi ya Jumapili ya sare ya 0-0 dhidi ya Wolfsburg baada ya kukosa kuhudhuria mkutano wa timu. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 ni mfungaji wa mabao mengi katika timu hiyo msimu huu baada ya kufunga mabao...

Neymar amnyima Cavani kuwa mfungaji bora wa muda wote wa PSG

Neymar alizomewa na mashabiki wa Paris St-Germain baada ya kumnyima Edinson Cavani fursa ya kuwa mchezaji aliyeifungia klabu hiyo mabao mengi wakati wa mechi dhidi ya Dijon. Bao la kipindi cha kwanza la Cavani lilimfanya kuwa sawa kwa magoli na mshambuliaji wa zamani Zlatan Ibrahimovic akiwa na magoli 156 katika mashindano yote aliyochezea PSG. Wenyeji hao waliongoza kwa 4-0 katika kipindi cha kwanza na Neymar alikuwa tayari amekamilisha hat-trick kabla ya PSG kupata penalti. Hatahivyo raia huyo wa Brazil aliamua kupiga mkwaju huo wa penalti badala ya kumwachia Cavani, hatua iliomfanya Neymar kuzomwa na mashabiki wa timu hiyo , lakini kocha Unai Emery alimtetea mchezaji huyo baada ya mechi hiyo. 'Nadhani Neymar alipiga mkwaju huo wa penalti kwa sababu ilikuwa siku nzuri kwake'', alisema Emery. ''Tunafurahia. Lakini kutakuwa na fursa nyingi kwa Cavani kufunga mabao zaidi''. Beki wa PSG Thomas Meunier aliitaja hatua hiyo ya Neymar kuwa aibu lakini akaong...

Simba yamtangaza kocha Mfaransa.

Klabu ya Simba leo imemtangaza rasmi Mfaransa Pierre Lechantre, kuwa Kocha mpya atakayekinoa kikosi hicho ambacho kilikuwa hakina mwalimu baada ya kumfukuza aliyekuwa kocha wake, Joseph Omog mwishoni mwa mwaka jana. Taarifa hiyo iliyotolewa na Msemaji Mkuu wa Klabu hiyo, Haji Manara imeeleza kuwa kocha huyo ataanza kazi mara moja na atasaidiwa na kocha msaidizi wa sasa Masoud Djuma ambae alikuwa akikaimu nafasi hiyo na Mfaransa huyo atashuhudia mchezo wa Simba SC dhidi ya Singida United leo Januari 18, 2018 katika Uwanja wa Taifa. Mfaransa huyo alishawahi kukinoa kikosi cha timu ya taifa ya Cameroon kilichoshinda ubingwa wa Afrika mwaka 2000 na ameshawahi kushinda tuzo ya kocha bora wa bara la Afrika 2001.

Alexis Sanchez kugharimu Manchester United

Ulidhani ni rahisi au ni bure kwa Alexis Sanchez kwenda Manchester United? Usijidanganye siyo bure hata kidogo, bali Manchester United watachomoka kiasi kikubwa sana cha pesa kwa mshambuliaji huyo. £180m United wataitumia katika dili la Sanchez na katika pesa hiyo kiasi cha £35m kinatajwa kama kiasi ambacho Arsenal watavuna endapo watakubali kumuuza Alexis Sanchez kwenda Manchester United. Kuna pesa nyingine ndefu sana ambayo ni £117m, kiasi hicho cha pesa United watatumia kumlipa mshahara Sanchez wakati wote atakapokuwa katika klabu hiyo na inatajwa kwamba mkataba wake atasaini miaka minne na nusu. Halafu kuna £20m hii inatajwa ni pesa ambayo Sanchez anaweza kuipata toka United kama akimwaga wino kuitumikia klabu hiyo na usisahau kwamba wakala wake naye atapewa kiasi cha £10m. Inatajwa kwamba United hawajali hata kidogo kuhusu pesa na wako tayari kutumia pesa yote hiyo kwa Alexis Sanchez ilimradi tu Sanchez asaini katika timu yao, usajili wa Sanchez unaonek...

Walcott ajiunga rasmi na Evarton

Everton imekamilisha usajili wa mshambuliaji wa Arsenal Theo Walcot katika mkataba ulio na thamani ya £20m katika kandarasi ya miaka mitatu na nusu. Walcott, 28, ni mchezaji wa pili kusajiliwa na mkufunzi wa Everton Sam Allardyce katika dirisha la uhamisho la Januari baada ya mshambuliaji Cenk Tosun aliyesajiliwa kwa dau la £27m kutoka Besiktas. Hatua hiyo inakamilisha huduma za Walcot za miaka 12 katika klabu hiyo ambapo alifunga magoli 108 katika mechi 397 "Kuna kitu muhimu kuhusu uhamisho huu najihisi vyema sana'', alisema Klabu ya zamani ya Walcott Southampton pia walikuwa na hamu ya kumsajili mchezaji huyo. Lakini Walcott, ambaye hajaanza mechi yoyote ya ligi ya Arsenal msimu huu anaamini kwamba Allardyce anaweza kuimarisha mchezo wake. ''Nilihisi kwamba ni wakati nilifaa kuondoka'', alisema. Ni uchungu lakini ni vyema na nataka kuimarisha mchezo wangu na kuisaidia Everton kushinda mataji kama ilivyokuwa awali. Aliongezea: Mkufunzi amekasirika ...

Mourinho na Manchester United kuafikiana mkataba.

Mazungumzo kati ya pande hizo mbili yanaendelea vyema na ni suala la muda tu kabla ya Mourinho hajaongeza mkataba mpya klabuni hapo na mkataba wake wa sasa unafikia ukingoni mwaka 2019. Taarifa za ndani ya klabu zinaeleza kuwa kama kocha huyo atasaini mkataba mpya utamuweka klabuni hapo mpaka mwaka 2021. Licha ya kulaumiwa na wachambuzi wengi wa soka pamoja na washabiki wa klabu ya Man kuwa timu hiyo inacheza mchezo wa kujilinda bado viongozi wa United wanaona kuwa Mourinho anaweza ibeba timu hiyo katika kuipa mataji makubwa barani Ulaya. Mourinho alijiunga na United mwaka 2016 kuchukua mikoba ya Luis Van Gaal, ameisadia Man United kutwaa ubingwa mwa kombe la Europa na Lile la EfL Carabao.

Tetesi za soka Ulaya Jumatano 17 Januari 2018

Chelsea wamezungumza na West Ham kuhusu kumsaini mshambuliaji wa miaka 29 Andy Carroll kwa mkataba wa kudumu. (Telegraph) West Ham wanataka kuskiliza ofa ya pauni milioni 20 kwa Carroll. (Sky Sports) Kiungo wa kati raia wa Armenia, Henrikh Mkhitaryan, 28, anasema anataka nyongeza ya mshahara kuweza kuhama Manchester United kwenda Arsenal. (Mirror) Kiungo wa kati wa Arsenal na England Jack Wilshere, 26, ambaye mkataba wake unakamilika msimu huu ni lazima afanyiwe uchunguzi wa kiafya na kukubali mshahara wake kupunguzwa kwa asilimia 20 kuweza kupata mkataba mpya. (Sun) Barcelona wamekataa ofa ya pauni milioni 22.2 kutoka Inter Milan kwa raia wa Brazil mwenye umri wa miaka 24 Rafinha kwa sababu wanataka pauni milioni 35.5. Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger ana wasi wasi kuhusu kumsaini mshambuliaji mwenye hasira wa Borussia Dortmund Pierre-Emerick Aubameyang. (Star) Tottenham ni kati ya vilabu vinavyommzea mate mchezaji wa hadhi juu wa Norwich James Maddison, 21. (London Evening Stan...

Ronaldinho astaafu soka rasmi.

Nyota wa zamani wa timu ya taifa ya Brazil na klabu za PSG, Barcelona na Ac Milan Ronaldo de Assis Moreira Maarufu kama Ronadinho Gaucho amestaafu soka. Licha ya Ronadinho kutocheza soka la kiushindani toka mwaka 2015 amekuwa akicheza michezo ya mabonanza Kaka na wakala wa mchezaji huyo Roberto Assis amethibitisha kuwa umefika mwisho kwa fundi huyo wa Brazil kucheza soka. Ronaldinho alianzia soka yake katika klabu ya Gremio ya nchini kwao kabla ya kujiunga na Paris St-Germain mwaka 2001 na baadaye kujiunga na Barcelona alikong'ara sana. Katika msimu wa 2010 -2011 alijiunga na AC Milan ya Italia kabla ya kurudi kwao na kujiunga na Flamengo mwaka 2011. Kisha alichezea vilabu vya Atletico Mineiro, na Queretaro ya nchini Mexico na kurudi tena kwao Brazil katika klabu ya Fluminense.

Ronaldo kafulia au ni mpito tu?

Msimu wa 2005-2006 ulikuwa msimu wa mwisho kwa CR7 kuumaliza akiwa na mabao machache zaidi katika ligi, msimu huo Cristiano Ronaldo alicheza michezo 33 lakini akamaliza akiwa na mabao 9 tu. Hii leo ni tarehe 15 January 2018 raundi ya pili ya La Liga Cristiano Ronaldo ana mabao 4 tu, tangu ajiunge na Real Madrid hajwahi kufika wakati kama huu akiwa na idadi ndogo ya mabao kiasi hicho. Msimu wa mwaka 2014/2015 wakati kama huu mwezi wa kwanza tayari CR7 alikuwa ameshacheka na nyavu mara 28 lakini sasa anahangaika na wastani unaonesha anafunga bao moja kila baada ya dakika 311, rekodi mbovu zaidi kwake. Mbaya zaidi kwa Cr7 hajawahi kuachwa kiasi hichi na mpinzani wake Lioneil Messi kwa idadi ya mabao katika kipindi  kama hiki, Messi ana mabao 16 hadi sasa ikiwa ni tofauti ya mabao 12 na alipo CR7. Lakini hilo ni La Liga tu ila huko kwingineko katika Champions League kama kawaida yake Mreno huyo anaendeleza uswahiba wake na nyavu ambapo michezo yake 6 ana mabao 9, lakini kwa umri wa...

Hakuna makubaliano au maombi ya Mikhitaryan au Aubameyang kwenda Arsenal

Hakuna makubaliano yaliofikiwa kwa mshambuliaji wa Manchester United Henrikh Mkhitaryan kujiunga na Arsenal ili kuwa mbadala wa Alexis Sanchez, kulingana na duru iliokaribu na Mkhitaryan. Inaaminika kwamba Sanchez ameingia katika makubaliano ya kibinafsi na United. Lakini man United na Arsenal haziwezi kuafikiana makubaliano yoyote bila Mkhitaryan kwenda Arsenal. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 anaaminika kutathmini mpango huo na hana haraka ya kutoa uamuzi wa mwisho. United iliipiku Arsenal katika kumsajili Mkhitaryan kutoka klabu ya Borussia Dortmund kwa dau la £26m mnamo mwezi Julai 2016. Hataki kutoka Old Trafford kwa lolote lile lakini ana wazo tofauti na lile la Jose Mourinho na hatua hiyo imeongeza uwezekano wa yeye kuondoka. Inadaiwa kuna sababu nyengine mbadala katika meza na hilo haliondoi dhamira yake ya kutaka kusalia Man United ambapo amepewa kandarasi ya hadi 2020. Pia inaaminika kwamba Dortmund imakataa kuwasilisha ombi la kutaka kumsajili tena Mkhitary...

Tetesi za soka Ulaya Jumanne 16 Januari 2018

Arsenal wako kwenye mazungumzo kumsani mchezaji wa Borussia Dortmund na Gabon Pierre-Emerick Aubameyang kuchukua mahala pake Alexis Sanchez. (Mirror) Arsenal wako mbioni na pauni milioni 53 kumpata Aubameyang 28. (Mail) Na Jose Mourinho anasema kuwa hana ukakika kuwa atamleta Sanchez huko Manchester United. (Mirror) Chelsea pia wamejiunga katika mbio za kumpata Sanchez lakini United wana uhakika kuwa kumpeana Henrikh Mkhitaryan, 28, kama sehemu ya makubaliano inawaweka katika nafasi nzuri. (Telegraph) Mshambuliaji wa Real Madrid na Ureno Cristiano Ronaldo, 32, anataka kurudi Manchester United. (As.com - in Spanish) Kiungo wa kati Emre Can, 24, anasema kuwa hajasaini makubaliano ya kujiunga na Juventus msimu huu na bado anazungumza na Liverpool kuhusu kuendelea kubaki huko Anfield. (Times - subscription required) Swansea City wamefanya mazungumzo na Atletico Madrid kuhusu makubaliano ya kuwaleta mshambuliaji wa raia wa Ufaransa Kevin Gameiro 30, na mBrazil Nicolas Gaitan, 29, huko...

Atletico Madrid kufungua mashtaka dhidi ya Fc Barcelona

Atletico Madrid wanajiandaa kufungua kesi rasmi FIFA kuhusu suala la Barcelona kuanza mazungumzo kinyume na sheria na mchezaji wao Antonie Griezmann. Mapema wiki hii iliripotiwa kwenye vyombo vya habari za Hispania kwamba Rais wa Barcelona Josep Maria Bartomeu hivi karibuni alikutana na wazazi wa Griezmann na kuongelea uhamisho wa mchezaji huyo kwenda Nou Camp. Na kwa mujibu wa taarifa kutoka mtandaonwa AS, Atletico Madrid watairipoti Barcelona kwa mchezo wao mchafu wanaofanya kumsaini mshambuliaji huyo wa Ufaransa. Atletico wanalalamika kwamba wanaondoa uaminifu kwenye masuala ya uhamisho kwa kujaribu kumsaini Griezmann kinyume na sheria kutoka wapinzani wao wa ligi. Barca wanaongoza ligi, huku Atletico wakiwa nyuma yao kwa pointi 6 kwenye nafasi ya pili. Uamuzi wa kuishtaki Barcelona ulifikiwa katika kikao cha wawekezaji mnamo Jumatatu iliyopita, japokuwa kuna urafiki mkubwa kati ya CEO Gil Marin na Rais wa Barca Josep Bartomeu. Griezmann amekuwa akihusishwa sana na uhamisho wa...

Messi afikia rekodi ya Gerrard Muller

Siku ya jana jumapili katika mechi ya la Liga mshambuliaji Lionel Messi aliifungia timu yake ya Fc Barcelona goli dhidi ya Levante Bao hili limemfanya Lionel Messi kuandika rekodi mpya ya mabao 365, ni Gerrad Muller pekee ambaye amewahi kufunga mabao 365 katika ligi moja barani Ulaya na sasa Messi anakuwa amemfikia Muller. Hii ina maana kama Lionel Messi atafunga bao moja tu katika michezo aliyobakisha kucheza baasi nyota huyu wa Kiargentina atakuwa mchezaji wa kwanza barani Ulaya kufunga mabao 366 katika ligi moja. Lakini wakati Messi akiifikia rekodi ya Gerrard Muller,  pia mchezaji huyo alifikisha jumla ya michezo 400 akiwa na klabu ya Barcelona, katika michezo hiyo 400 Messi amefanikiwa kufunga mabao 365 na kutoa assist 142 akibeba makombe 30. Wakati Lioneil Messi akifanya hayo, pacha wake uwanjani ambaye ni Luis Suarez naye amefanikiwa kufikisha mabao 132 akiwa na La Liga na sasa anakaa juu ya Samuel Etoo mwenye mabao 131

Tetesi za soka Ulaya Jumatatu 8 Januari 2018

Mshambuliaji wa Ufaransa Antoine Griezmann, 26, ataitisha pauni 400,000 kwa wiki kuzuia ofa ya Chelsea ili kujiunga na Manchester United. (Sun) Chelsea wanamtaka mshambuliaji wa Borussia Monchengladbach na Ubelgiji Thorgan Hazard, 24, kujiunga na ndugu zake Eden, 27, na Kylian, 22, huko Stamford Bridge. (Bild - in German) Liverpool wanamtaka mshambuliaji wa Monaco na Ufaransa Thomas Lemar, 22, kuchukua mahala pake Philippe Coutinho - na wanataka kufanya hilo wiki hii. (Mirror) Manchester United na Chelsea zimemuulizia mshambuliaji wa Porto Mousa Marega, 26. (Metro) Real Madrid walikuwa na nia ya kutoa ofa ya pauni milioni 177 kwa Coutinho kabla ya kukubali kujiunga na Barcelona kwa pauni milioni 142. (Mundo Deportivo - in Spanish) Coutinho atafanyiwa uchunguzi wa kiafya leo Jumatatu na kutangazwa rasmi kama mchezaji wa Barcelona lakini kuanza kwake kucheza kunaweza kucheleweshwa kutokana na jeraha. Nyota wa Barcelona Lionel Messi ametaka Philippe Coutinho kuwepo katika kikosi cha...

Ndoto za Coutinho zatimia baada ya kutua Barca

Kiungo wa kibrazil Philippe Coutinho amesema uhamisho wake kwenda Barcelona ni ndoto iliyokamilika. Kiungo huyo alieleza hisia zake za kutimiza ndoto yake alipokuwa akipigwa picha katika uwanja wa Nou Camp wakati klabu yake mpya ilipokuwa ikicheza na Levante. "Mashabiki wa Barcelona tayari nipo hapa, ndoto zimekuwa kweli natumani tunaonana kesho, " alisema Coutinho kupitia video fupi aliyoiweka katika mtandao wa Twita. kuwa mchezaji mpya wa Barcelona baada ya klabu yake ya Liverpool kukubali kuuza kiungo huyo kwa dau la pauni milioni 142. Nyota huyu atasaini mkataba wa miaka mitano na klabu itayotaka kumnunu mchezaji huyo italazimika kutoa kiasi cha pauni milioni 355.

Philippe Coutinho atua Barca rasmi

Usajili wa Mbrazili Philippe Coutinho kutoka Liverpool kwenda Barcelona umekamilika kwa ada ya €160 Kwa sasa Philippe Coutinho ni mchezaji wa tatu ghali duniani. Taarifa kutoka Hispania zinadai kuwa Coutinho amechangia kiasi cha €15m

Conte na Mourinho katika bifu la kupanga matokeo

Meneja wa Manchester United Jose Mourinho ameendeleza vita ya meneno dhidi ya bosi wa Chelse Antonio Conte, akikumbushia adhabu ya Muitaliano huyo 2012 kwa kupanga matokeo. Mameneja hao wawili wameingia kwenye mgogoro siku mbili zilizopita Conte akisema kuwa Mourinho ana tabia ya "utovu wa nidhamu pembezoni mwa chaki". Msemo huo wa Conte aliutoa akimjibu Mourinho aliyebwata kuwa baadhi ya mameneja wa Premier League wana tabia "kama kijana chizi" wakati wa mechi - kauli ambayo ilimlenga bosi wa Chelsea. Muitaliano huyo alidai kuwa Mourinho alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa mbaya wa kupoteza kumbukumbu, akitaja kwa msamiati wa Kiitaliano akimlenga bosi wa Man United. "Nadhani anahitaji kujichunguza alivyokuwa huko hapo awali - labda alikuwa akijizungumzia alivyokuwa siku za nyuma," alisema Conte. "Labda, wakati mwingine, nadhani anasahau alichowahi kusema zamani, jambo ambalo ni tabia yake. "Wakati mwingine nadhani analo tatizo, silijui jina, la...

Tetesi za soka Ulaya Jumamosi 6 Januari 2018

Mafanikio ya Mohamed Salah mapema msimu huu akiwa Liverpool yameifanya Real Madrid kuvutiwa naye, kwa mujibu wa OK Diario. Vijana wa Zinedine Zidane wameshindwa kufanya maajabu mbele ya goli na wanatafuta utatuzi wa tatizo hilo, mchezaji huyo wa kimataifa wa Misri anapewa nafasi kubwa kutua Bernabeu. Madrid wanatambua kuwa kukamilika kwa dili hilo kwa uhamisho wa Januari ni vigumu kwa hiyo wanajipanga kwa ajili ya majira ya joto. Guangzhou Evergrande wamefikia makubaliano na Pierre-Emerick Aubameyang na Borussia Dortmund ya uhamisho wa mchezaji huyo wa kimataifa wa Gabon majira ya joto, kwa mujibu wa Sima Sports. Klabu hiyo ya Chinese Super League italazimika kutoa kitita cha €72 milioni kuhakikish mshambuliaji huyo anatua Beijing, wakiwa wameshatoa dau la €60m. Meneja w Arsenal, Arsene Wenger hajakataa uwezekano wa Alexis Sanchez kuondoka, na ikiwa mchezaji huyo wa Chile ataondoka kwenda Man City Januari, atakuwa tayari kumsajili Thomas Lemar wa Monaco kuwa mrithi wake...

Chelsea wafanikiwa kumsajili Barkley

Klabu ya Chelsea imefanikiwa kumsajili kiungo wa Everton, Ross Barkley siku ya Ijumaa. Uongozi wa klabu ya Chelsea umetangaza kuwa wamemsajili kiungo huyo kwa dau la pauni milioni 15. Ikumbukwe kuwa Chelsea walimkosa kiungo huyo katika dirisha kubwa la usajili lililopita.

Tetesi za soka Ulaya Ijumaa 5 Januari 2018

Arsenal wataangalia uwezekano wa kumsajili mshambuliaji wa Borussia Dortmund Pierre Emerick Aubameyang ikiwa Alexis Sanchez ataondoka uhamisho wa Januari kwa mujibu wa Gianluca Di Marzio . Alexis Sanchez bado yupo kwenye rada za Manchester City kwani mkataba wake unazidi kuelekea ukiongoni Emirates. Na Gunners wameshaanza kufanya mipango ya kutafuta mbadala wake, Aubameyang akipewa kiapumbele. Kocha mkuu wa Monaco, Leonardo Jardim amesisitiza kuwa Thomas Lemar hataondoka klabuni hapo uhamisho wa Januari. Mchezaji huyo amekuwa shabaha ya muda mrefu ya Liverpool na Arsenal, lakini Jardim amesisitiza kuwa Lemar hataondoka Monaco hadi majira ya joto. "Monaco haina tabia ya kuuza wachezaji majira ya baridi. Ni mkakati wetu. Wachezaji wanaelewa na wanafahamu jinsi mambo yanavyokwenda hapa", alisema Jardim. Manchester City wapo tayari kutoa kitita cha paundi milioni 35 kwa ajili ya kumsajili mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez kwa mujibu wa DailyMail .

Mohamed Salah ashinda tuzo ya mchezaji bora Afrika

Mohamed Salah amempiku mchezaji mwenzake wa Liverpool Sadio Mane na mshambuliaji wa Borussia Dortmund Pierre-Emerick Aubameyang kutwaa tuzo ya Mchezaji wa Afrika wa mwaka 2017. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Misri aliibuka mshindi katika kinyang'anyiro hicho dhidi ya wachezaji wenzake katika mkutano wa Tuzo za Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika mjini Accra. Salah, ambaye ataikosa mechi ya Kombe la FA raundi ya tatu dhidi ya Everton Ijumaa usiku, amefurahia mwaka wa mafanikio kwa klabu na kwa taifa lake pia. Baada ya kufunga mara 10 akiwa Roma kati ya Januari na Mei, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 aijiunga na Liverpool kwa uhamisho wa rekodi kwa klabu hiyo na kwa haraka ameshafanikiwa kuweka kimiani magoli 24 katika michuano yote. Akiongea kuelekea hafla hiyo, Salah aliwaambia waandishi: "Nadhani tuna timu bora ya taifa na tumefanya vizuri kwenye Kombe la Afrika na kufuzu Kombe la Dunia." Salah pia alizifumania nyavu mara mbili katika ushindi wa Misri wa 2-1 dh...

Kumbe Van Dijk alikuwa muosha sufuria

Safari ya mafanikio mara zote huwa ni ngumu sana, huwa sio rahisi kufikia kilele cha mafanikio kirahisi rahisi na hii ndio imemtokea pia mlinzi mpya wa Liverpool aliyenunuliwa toka Southamoton Virgil Van Djik. Djik kwa sasa amekuwa habari kubwa ya dunia baada ya rekodi ya usajili aliyoweka, kwa sasa Van Djik ndio mlinzi ghali duniani akinunuliwa kwa £75m huku kwa mwaka akiweka kwenye account kiasi cha £10m. Akiwa kijana mdogo wa miaka 16 Djik alikuwa hana kitu mfukoni na ilimfanya Djik kutafuta kazi ili kujiendeleza kimaisha na ndipo hapo aliamua kufanya kazi ya kuosha vyombo nchini kwao Uholanzi. Katika mji anaotokea wa Brenda alifanya kazi hii kwa ujira mdogo sana huku wafanyakazi wenzake wakimuambia asahau kuhusu soka ni ngumu kutoka akiwa huko bali aendelee na kazi ya kuosha masufuria. Djik hakutaka kusikia la mtu kwani aliamini soka ndio kitu chake cha kumtoa na sasa hadi mmiliki wa mgahawa ambao Djik alikuwa akifanyia kazi haamini kwamba mfanyakazi wake wa zamani ame...

Sanchez akubali kujiunga na Manchester City

Mshambuliaji wa kimataifa wa Chile anayekipiga katika klabu ya Arsenal ya Uingereza, Alexis Sanchez anatajwa kuwa amekubali kujiunga na klabu ya Manchester City. Mwandishi mmoja wa habari ambaye ni rafiki mkubwa wa mwanasoka huyo amesema jana kwamba ameambiwa “laivu” na Sanchez kwamba anaondoka rasmi na chaguo lake ni Manchester City. Gerard Romero ambaye ni mwandishi wa habari raia wa Hispania amesema kwamba ameambiwa na sanchez kwamba anakwenda Man City ili kuungana na kocha wakw wa zamani Pep Guardiola. Arsenal imekuwa kwa muda mrefu sasa ikihaha kumbakiza mchezaji huyo katika kikosi chake, lakini kwa tarifa hizo mpya ni kama vile jitihada hizo zimekwama. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 28 amekuwa na msimu bora katika Arsenal chini ya kocha wake, Arsene Wenger na ametumbukiza kambani mabao 30 katika mechi zote za mashindano. Hata hivyo, winga huyo yuko nje ya mkataba msimu ujao na kama anaondoka kwenda Man City maana yake anaondoka akiwa kama mchezaji huru. Na kwa mu...

Ronaldo kulipwa £600,000 kwa wiki

  Imeripotiwa kuwa Real Madrid wamefikia maamuzi ya kumlipa Cristiano Ronaldo ujira wa paundi £600,000 kwa wiki Katika nusu ya kwanza ya msimu, Ronaldo amefunga mara nne tu kwenye michuano ya La Liga na ameendelea kuhusishwa na tetesi za kutaka kujiunga na aidha Manchester United au Paris Saint-Germain. Hata hivyo, kwa mujibu wa Corriere Dello Sport, Real bado wanatamani kuendelea kumbakishia Ronaldo Bernabeu na wamejipanga kuupandisha mshahara wake kuwa sawa na wa Lionel Messi wa Barcelona na Neymar wa Paris Saint-Germain. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32 sasa bado amebakiwa na miaka minne na nusu kwenye mkataba wake, lakini Real wanaamini kumwongeza dau mchezaji huyo ku

Tetesi za soka Ulaya Alhamisi 4 Januari 2018

Mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez amekubali kwa maneno ya kinywa kujiunga na Manchester City, kwa mujibu wa Marca . Mchezaji huyo wa kimataifa wa Chile alikaribia kujiunga na City msimu wa majira ya joto na inaonekana anataka kumaliza mkataba wake ambao utaisha mwisho wa msimu huu Emirates. Inter wanataamani kumsajili kiungo wa Manchester United Juan Mata, kwa mujibu wa Daily Mirror . Muhispania huyo atakuwa amemaliza mkataba wake Old Trafford ifikapo mwisho wa msimu huu, ingawa anayo fursa ya kuongeza mkataba wake kwa mwaka mmoja zaidi. Manchester United wameanza kuhofu kuwa Jose Mourinho anaweza kujiuzulu kazi mwisho wa msimu huu kwa mujibu wa Daily Mail . Kocha huyo wa zamani wa Chelsea amekuwa katika kipindi kigumu wiki za hivi karibuni baada ya timu yake kujikuta nyuma ya Manchester City kwa pointi 15 katika mbio za ubingwa na ameweka bayana hadharani kuwa United hawajatumia fedha za kutosha kuwa washindani.

Dembele kurejea dimbani.

Mchezaji aliyenunuliwa pesa nyingi zaidi na Barcelona Ousmane Dembele huenda akarejea kucheza wiki hii baada ya kukaa nje ya uwanja wa karibu miezi minne. Mshambuliaji huyo wa Ufaransa mwenye miaka 20 alijiunga na Barca Agosti kwa £96.8m lakini akaumia akichezea klabu hiyo mechi yake ya tatu - dhidi ya Getafe mnamo 16 Septemba. Dembele alifanyiwa upasuaji nchini Finland. Sasa, huenda akarejea kucheza dhidi ya Celta Vigo katika Copa del Rey Alhamisi. Viongozi wa ligi Barcelona kisha watakutana na Levante katika La Liga Jumapili. Barca ambao wamo alama tisa mbele kileleni kwenye ligi wamepangiwa kukutana na Chelsea hatua ya 16 bora Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya Februari na Machi. Dembele - aliyejiunga nao kutoka Borussia Dortmund - ndiye mchezaji wa pili ghali zaidi duniani ba bei yake ya uhamisho inaweza kupanda hadi £135.5m. Pesa walizolipa Barcelona mwanzoni zilikuwa karibu nusu ya £200m walizopokea kutoka Paris St-Germain kwa mshambuliaji Mbrazil Neymar .

Tetesi za soka Ulaya Jumatano 3 Januari 2018

Sergio Aguero ametoa dondoo kuwa anaweza kuondoka Manchester City mwishoni mwa msimu huu. Goal iliripoti mwezi Desemba kuwa Mwargentina huyo hana furaha katika klabu hiyo msimu huu baada ya kuachwa benchi mara nyingi na Pep Guardiola. Na ingawa hataki kuondoka, amekiri kuwa klabu ndiyo yenye tamko la mwisho kwenye mustakabali wake. Philippe Coutinho ameendelea kusisitiza kuwa anataka kuihama Liverpool ili ajiunge na Barcelona Goal imabaini. Real Madrid wanataka kuvunja mkataba wa Kepa Arrizabalaga ili kuipata saini ya mlinda mlango huyo wa Athletic Club, kwa mujibu wa Marca . Athletic hata hivyo hawana mpango wa kumuuza kipa huyo wa kimataifa wa Hispania, lakini Mabingwa hao wa Ulaya wanataka kutumia nguvu yao ya mshiko kumpata. Real Madrid wapo tayari kumuuza Toni Kroos kwa Manchester United ikiwa ni sehemu ya jitihada zao kupata fedha ya kumsajili Neymar kutoka PSG kwa mujibu wa The Express . West Ham wapo tayari kutoa kitita cha £15 milioni kumsajili Joe Allen kutoka Stok...

Conte: Chielin wa nini?

Kocha mkuu wa Chelsea Antonio Conte amefutilia mbali madai kuwa ana mpango wa kumsajili beki wa Juventus Giorgio Chiellini Conte yupo sokoni kwa ajili ya kutafuta wachezaji wachache katika dirisha la uhamisho wa Januari na David Luiz amekuwa akihusishwa na tetesi za kuwa mbioni kuondoka Stamford Bridge, Chiellini akitajwa kuwa miongoni mwa wanaweza kuirithi nafasi yake. Hata hivyo, licha ya kuwahi kufanya kazi na Muitaliano huyo hapo awali, Conte anasema kuwa hajafikiria kumleta Chiellini Premier League. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 48 sasa aliwaambia waandishi: "Kwenye soko la uhamisho kuna tetesi. Sisi tutafanya kilicho chema kwa ajili ya timu. "Ni lazima niwe mkweli. Giorgio ni mchezaji shupavu na bora lakini anataka kumalizia soka lake Juventus. Ni sahihi kumaliza soka kwa namna hii." Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 33 amedumu Turin kwa muda wa miaka 12 na nusu, akicheza jumla ya mechi 453 katika michuano yote.

Kwaheri Coutinho

Philippe Coutinho amecheza mechi yake ya mwisho kwa klabu ya Liverpool kwani anatazamia kwenda Barcelona kwa mujibu wa habari Miamba wa Catalan wamekuwa wakimfukuzia kwa muda mrefu Coutinho lakini walikwama wakiwa wametoa ofa tatu ambazo zilikataliwa kwa ajili ya Mbrazili huyo majira ya joto. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 ameweka bayana kuwa alitaka kutua Camp Nou, na kuiomba Reds kumruhusu kuondoka, lakini klabu hiyo ilisisitiza kuwa mchezaji wao nyota haendi popote. Hata hivyo, Daily Mail limedai kuwa Liverpool imebadili mtazamo na sasa wapo tayari kuachana na mchezaji huyo wa zamani wa Inter Milan, ambaye kwa sasa ni majeruhi. Ripoti zinaendelea kudai kuwa ofa isiyopungua £133m tu ndiyo itakayoweza kuishawishi Liverpool kufanya biashara hiyo katika dirisha la uhamisho kipindi hiki kumuuza mchezaji ambaye bado alikuwa muhimu kwao kutokana na kiwango chake matata. Coutinho amecheza mechi 20 Liverpool katika michuano yote msimu huu, akifunga magoli 12 na kutengeneza me...

Everton wachapwa live mbele ya Rooney

Mchezo huo wa Premier League ulipigwa nyumbani kwa Everton kwenye Uwanja wa Goodison Park ambapo licha ya kuongozwa na Wayne Rooney bado timu hiyo ilishindwa kufurukuta. Mabao ya Man United katika mchezo huo yalifungwa na Anthony Martial katika dakika ya 57 na Jesse Lingard katika dakika ya 81. Kutokana na matokeo hayo Man United imerejea nafasi ya pili kutoka ya tatu kwa kuwa na pointi 47 huku Chelsea ikifuatia kwa kuwa na pointi 45 licha ya kuwa yenyewe ipo nyuma mchezo mmoja na inatarajiwa kucheza na Arsenal, kesho Jumatano.

Guardiola: Sanchez atabaki Arsenal.

Pep Guardiola anatarajia Alexis Sanchez atabaki Arsenal Januari licha ya kocha huyo wa Manchester City kubashiri kuwa Gabriel Jesus atakuwa nje kwa muda usiopungua miezi miwili. Nyota huyo wa kimataifa wa Chile, ambaye anaingia kwenye miezi sita ya mwisho kwenye mkataba wake, alihusishwa na tetesi za kutua City mwanzo wa msimu na alikuwa karibu kuondoka Emirates kabla ya dirisha la usajili kufungwa. Na baada ya Jesus kupata majeraha, Guardiola anatarajia Mbrazili huyo atakuwa nje ya dimba kwa muda wa takribani miezi mwili baada ya sare ya 0-0 dhidi ya Crystal Palace, Bosi huyo wa zamani wa Barcelona aliukuzwa kama habari hizo zinaweza kumlazimu kumsajili mara moja mchezaji huyo wa zamani wa Barcelona. Lakini Guardiola hadhani kama Sanchez ataondoka Arsenal ndani ya wiki chache zijazo. "Sijui," aliwaambia waandishi alipoulizwa ikiwa Sanchez atakuwa kwenye nafasi nzuri kutua City. "Ni mchezaji wa Arsenal na nadhani ataendelea kubaki pale. Tutakuwa na mkutano wa ndani ...

Tetesi za soka Ulaya Jumanne 2 Januari 2018

Jose Mourinho amepania kusimamisha mipango yote kuhakikisha anamsajili mshambuliaji wa Atletico Madrid Griezmann, kwa mujibu wa the Daily Star. Ingawa mpango ulikuwa kumsajili majira ya joto, lakini baada ya Romelu Lukaku na Zlatan Ibrahimovic kupata majeraha mabadiliko ya haraka yanahitaji kufanyika. Real Madrid inataka kuachana na mpango wa kuifukuzia saini ya mshambuliaji wa Chelsea Eden Hazard, kwa mujibu wa Marca . Badala yake Zinedine Zidane anajipanga kumpa nafasi kijana wake wa miaka 23 Marco Asensio kwani anamini Mbelgiji huyo ataua maendeleo ya Muhispania huyo. Mauro Icardi anatamani kutua Manchester United ikiwa ataondoka Inter Milan, kwa mujibu wa Don Balon . Pamoja na kwamba Icardi amejidhatiti kuisaidia klabu yake katika mbio za taji la Serie A, bado anaangalia mustakabali wake.