Uongozi wa klabu ya Mamelody Sundowns ya Afrika Kusini umethibitisha rasmi kuwepo kwa mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya mabingwa wa Uhispania Barcelona. Mchezo huo utachezwa Mei 16 katika Uwanja wa FNB ikiowa ni sehemu ya maadhimisho ya kusherekea miaka 100 tangu kuzaliwa kwa rais wa kwanza wa taifa hilo, Nelson Mandela. Hii itakuwa mara ya pili kwa klabu hizo kucheza nchini Afrika Kusini, mara ya kwanza ilikuwa 2007 ambapo Barcelona ilishinda mabao 2-1. Awali chama cha soka nchini Afrika Kusini, SAFA kilibariki uwepo wa mchezo huo baada ya mkutano na waandishi wa habari uliofanyika Jumanne. Mbali na Mamelod, mchezo huo unaandaliwa pia kwa ushirikiano na Serikali ya Afrika Kusini, Mfuko wa Patrick Motsepe na Mfuko wa Nelson Mandela.
Zikiwa zimebaki mechi mbili msimu wa 2017/18 wa La Liga kumalizika, Real Madrid wana pointi 72 na endapo watashinda mechi zao zote wataishia kupata pointi 78 tu. Msimu wa mwisho Real Madrid kupata pointi chache zaidi kwenye La Liga, ulikuwa msimu wa 2008/09 - ambapo Los Blancos wakiwa chini ya Juande Ramos, hawakushinda taji lolote, wakiwaangalia Barcelona chini ya Pep Guardiola wakishinda mataji matatu na kuwafunga Madrid 6-2 nyumbani kwao Bernabeu. : Msimu huu mambo yanaweza kuwa tofauti, Madrid wapo kwenye fainali ya ulaya na endapo watashinda watakuwa wamefanikiwa kimataifa lakini watakuwa wamefeli nyumbani tena - mpaka hivi sasa wapo nyuma kwa pointi 18 nyuma ya Wakatalunya ambao tayari wameshabeba ubingwa. Leo usiku Madrid atakuwa akiumana na Celta Vigo