Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tetesi za soka Ulaya Jumapili 26.11.2017

Mshambuliaji wa Real Madrid na Ureno Cristiano Ronaldo, 32, amefanya mazungumzo ya siri na PSG (DiarioGol, in Spanish)

Alan Pardew anatarajiwa kuteuliwa kuwa mkufunzi mpya wa West Brom na inatarajiwa kwamba mkufunzi huyo wa zamani wa Crystal Palace huenda akaanza kazi siku ya Jumatatu.. (Sun)

Kiungo wa kati wa Ujerumani na Arsenal Mesut Ozil, 29, atapewa mkataba wa dau la £350,000 kwa wiki ili kuhamia Barcelona (Daily Mirror)

Lakini mkufunzi wa Arsenal Arsene Wenger amekana kwamba hakuna mazungumzo yoyote ya Ozil kuondoka katika klabu hiyo ya uwanja wa Emirates (Daily Star)

Mkufunzi Antonio Conte anaitaka Chelsea kusuluhisha swala la kandarasi mpya ya kipa Thibaut Courtois. (Guardian)

Vyombo vya habari vya Ubelgiji vinadai kwamba Courtois, 25, anataka kulipwa Yuro 230,000 kwa wiki (£205,000) ili kupata mshahara sawa na kipa David de Gea katika klabu ya Manchester United. (HLN, in Dutch)

Mkufunzi wa zamani wa West Brom Tony Pulis anaongoza orodha ya wachezaji wanaotarajiwa kuchukua wadhfa wa ukufunzi katika klabu ya Swansea City iwapo mkufunzi Paul Clement atafutwa. (Daily Mail)

Kiungo wa kati wa Liverpool Emre Can, 23,ameripotiwa kukubali kandarasi na klabu ya ligi ya serie A Juventus (Tuttosport, via Daily Star)

Fiorentina imeingia katika mbio za kutaka kumsajili mshambuliaji wa Everton mwenye umri wa miaka 20 Henry Onyekuru, ambaye yuko kwa mkopo katika klabu ya Anderlecht. (Sun)

Kiungo wa kati wa Arsenal Jack Wilshere, 25, anasema kuwa atajadiliana kuhusu uhamisho na mkufunzi Arsene Wenger wakati dirisha la uhamisho la mwezi Januari litakapofunguliwa katika kipindi cha wiki chache zijazo kwa kutochezeshwa katika ligi ya Uingereza. (Daily Express)

Mwenyekiti wa Everton Farhad Moshiri amewaorodheshwa wakufunzi watatu na ametangaza kuwa hivi karibuni watamuajiri kocha wa klabu hiyo.(Reuters)

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Nitapindua dunia juu chini ili kubaki kama meneja wa Arsenal

Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake. Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal Kazi yake katika timu hiyo iliwekwa utatani wakati alipokataa kudhibitsha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror) Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)

Robert Lewandowski mfungaji bora Bundesliga 2017/2018

Robert Lewandowski amemaliza msimu wa 2017/18 wa Bundesliga akiwa mfungaji bora kwa mara ya 3 kwenye maisha yake ya soka. : • 30 games • 29 goals

Je Barcelona wataweza kuvunja rekodi hizi?

Hadi sasa miamba  ya Catalunya Fc Barcelona haijapoteza mchezo hata mmoja katika ligi kuu nchini Hispania na wanaonekana wanaweza kuweka rekodi ya kuwa timu pekee kumaliza La Liga bila kupoteza, lakini je na haya yafuatayo wataweza? Magoli 121, Jose Mourinho msimu wa 2011/2012 alimaliza La Liga akiwa na mabao 121, hadi sasa Barcelona wana mabao 70 na itawabidi kufunga mabao 51 katika mechi zao 11 zilizobaki ili kuifikia rekodi ya Mourinho. Zamora award, hii ni tuzo ya kipa aliyefungwa mabao machache, Francisco Liano mlinda lango wa zamani wa klabu ya Sporting Gijon anashikilia rekodi ya kufungwa mabao machache zaidi La Liga, mabao 18 (1993/1994). Hadi sasa mlinda lango wa Atletico Madrid Jan Oblak ameruhusu mabao 12 katika lango lake huku golikipa wa Barcelona Marc Andre Stegen akiwa ameruhusu mabao 13 hadi sasa, na anasubiriwa kati ya hawa nani atavunja rekodi ya Liano. Real Sociedad record, Barcelona hawajapoteza katika michezo 32 ya La Liga na wamevunja rekodi ya Pep G...