Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tetesi za usajili Ulaya

Miamba ya soka kutoka London, Chelsea wako mbioni kumsajili mshambuliaji wa Borussia Dortmund, Pierre Emerick Aubameyang ambaye anaonekana kutokuwa na moyo wa kuichezea klabu hiyo tena.
Klabu ya Borussia Dortmund imeziarifu baadhi ya timu kuwa atakuwa sokoni Januari mwakani.

Klabu za Arsenal na Liverpool ziko katika upinzani wa kumnyakua winga wa PSG Julian Drexler. Liverpool wamekuwa wakimuhitaji winga huyo kwa mkopo lakini PSG wamesisitiza kuwa anauza. Pia ikumbukwe kabla ya Draxler kwenda PSG alikuwa akihitajika na washika bunduki wa London.

Pia klabu ya FC Barcelona bado wanajiandaa kumnasa kiungo wa klabu ya Tottenham katika dirisha dogo la usajili. Miamba hiyo inaami kuwa anaweza kuwa mbadala wa Andres Iniesta ambaye soka lake linaelekea ukingoni.

PSG wako mbele Manchester City katika mbio za kumuwania mshambuliaji wa klabu ya Arsenal Alexis Sanchez ambaye ana kila dalili za kuondoka klabuni hapo Januari mwakani. Mkataba wa mshambuliaji huyo wa Chile unafikia ukomo mwakani Januari.

Klabu ya Borussia Dortmund, inataka kumsajili mchezaji wake wa zamani Mikhitaryan anayekipiga huko Manchester United. Manchester United walimsajili mchezaji huyo kutoka Borussia Dortmund kwa dau la €30 milioni na sasa wako tayari kumsajili tena.

Ronaldo yuko tayari kwa mazungumzo na klabu ya PSG. Cristiano Ronaldo amemwambia wakala wake George Mendes afanye mazungumzo na viongozi wa klabu ya Paris Ufaransa. Mchezaji huyo wa Ureno anafanya hivyo ili kulazimisha mshahara mkubwa na anaamini PSG ndiyo wanaoweza kumtimizia mahitaji yake ya kifedha. Hii imekuja baada ya hasimu wake Lionel Messi kuongezewa mkataba mnono hadi mwaka 2021.

Kocha wa klabu ya Atletico Madrid, Diego Simeon anataka kumsajili kiungo wa PSG Javier Pastore, Pastore hana furaha na maisha ya klabuni PSG.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Nitapindua dunia juu chini ili kubaki kama meneja wa Arsenal

Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake. Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal Kazi yake katika timu hiyo iliwekwa utatani wakati alipokataa kudhibitsha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror) Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)

Robert Lewandowski mfungaji bora Bundesliga 2017/2018

Robert Lewandowski amemaliza msimu wa 2017/18 wa Bundesliga akiwa mfungaji bora kwa mara ya 3 kwenye maisha yake ya soka. : • 30 games • 29 goals

Je Barcelona wataweza kuvunja rekodi hizi?

Hadi sasa miamba  ya Catalunya Fc Barcelona haijapoteza mchezo hata mmoja katika ligi kuu nchini Hispania na wanaonekana wanaweza kuweka rekodi ya kuwa timu pekee kumaliza La Liga bila kupoteza, lakini je na haya yafuatayo wataweza? Magoli 121, Jose Mourinho msimu wa 2011/2012 alimaliza La Liga akiwa na mabao 121, hadi sasa Barcelona wana mabao 70 na itawabidi kufunga mabao 51 katika mechi zao 11 zilizobaki ili kuifikia rekodi ya Mourinho. Zamora award, hii ni tuzo ya kipa aliyefungwa mabao machache, Francisco Liano mlinda lango wa zamani wa klabu ya Sporting Gijon anashikilia rekodi ya kufungwa mabao machache zaidi La Liga, mabao 18 (1993/1994). Hadi sasa mlinda lango wa Atletico Madrid Jan Oblak ameruhusu mabao 12 katika lango lake huku golikipa wa Barcelona Marc Andre Stegen akiwa ameruhusu mabao 13 hadi sasa, na anasubiriwa kati ya hawa nani atavunja rekodi ya Liano. Real Sociedad record, Barcelona hawajapoteza katika michezo 32 ya La Liga na wamevunja rekodi ya Pep G...