Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Wenger azitimulia vumbi Man Utd, Barca

Wenger yupo tayari kupambana na klabu za Barcelona na Manchester United kwa ajili ya kumnasa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20.
In the headlines Wenger azitimulia vumbi Man Utd, Barca
SUNDAY NOVEMBER 26 2017

LONDON, ENGLAND. KOCHA wa Arsenal Arsene Wenger ameamua kuanzisha mbio za kumsaka nyota wa Monaco na timu ya taifa Ufaransa Thomas Lemar katika dirisha la usajili la Januari mwakani.
Wenger yupo tayari kupambana na klabu za Barcelona na Manchester United kwa ajili ya kumnasa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20.
Mchezaji huyo kwa sasa ni habari ya mjini kutokana na kiwango chake anachokionyesha klabuni, na kinachovutia timu kubwa duniani ni kitendo chake cha kuipa ubingwa timu yake katika msimu uliopita.
Katika dirisha la usajili lililopita, Wenger alijaribu kumnasa mchezaji huyo na hata alitoa ofa ya Pauni 90 milioni katika siku ya mwisho ya dirisha la usajili kujaribu kuishawishi Monaco imwachie mchezaji huyo lakini ilishindikana. Lemar, ambaye alijiunga na Monaco mwaka 2015 akitokea Caen amekuwa akichezea kikosi cha kwanza cha Ufaransa kwa muda sasa na kocha Wenger anaamini ndio suluhisho pekee kwa kikosi chake baada ya kuondoka kwa Alexis Sanchez na Mesut Ozil, ambao wana kila dalili ya kuondoka klabuni hapo Januari mwakani.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Nitapindua dunia juu chini ili kubaki kama meneja wa Arsenal

Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake. Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal Kazi yake katika timu hiyo iliwekwa utatani wakati alipokataa kudhibitsha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror) Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)

Robert Lewandowski mfungaji bora Bundesliga 2017/2018

Robert Lewandowski amemaliza msimu wa 2017/18 wa Bundesliga akiwa mfungaji bora kwa mara ya 3 kwenye maisha yake ya soka. : • 30 games • 29 goals

Je Barcelona wataweza kuvunja rekodi hizi?

Hadi sasa miamba  ya Catalunya Fc Barcelona haijapoteza mchezo hata mmoja katika ligi kuu nchini Hispania na wanaonekana wanaweza kuweka rekodi ya kuwa timu pekee kumaliza La Liga bila kupoteza, lakini je na haya yafuatayo wataweza? Magoli 121, Jose Mourinho msimu wa 2011/2012 alimaliza La Liga akiwa na mabao 121, hadi sasa Barcelona wana mabao 70 na itawabidi kufunga mabao 51 katika mechi zao 11 zilizobaki ili kuifikia rekodi ya Mourinho. Zamora award, hii ni tuzo ya kipa aliyefungwa mabao machache, Francisco Liano mlinda lango wa zamani wa klabu ya Sporting Gijon anashikilia rekodi ya kufungwa mabao machache zaidi La Liga, mabao 18 (1993/1994). Hadi sasa mlinda lango wa Atletico Madrid Jan Oblak ameruhusu mabao 12 katika lango lake huku golikipa wa Barcelona Marc Andre Stegen akiwa ameruhusu mabao 13 hadi sasa, na anasubiriwa kati ya hawa nani atavunja rekodi ya Liano. Real Sociedad record, Barcelona hawajapoteza katika michezo 32 ya La Liga na wamevunja rekodi ya Pep G...