Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Yanga dhidi ya Ngoma

Yanga imechoshwa na visa na vituko vya mshambuliaji wake Mzimbabwe Donald Ngoma na sasa inapanga namna ya kumwajibisha
Klabu Yanga imepanga kumuwajibisha mshambuliaji wake raia wa Zambabwe Donald Ngoma, kwa kosa la kwenda kwao bila ruhusu ya klabu hiyo ambayo anaitumikia kwa msimu wa tatu sasa.
Chanzo cha bari kutoka ndani ya klabu hiyo kimeiambia Goal , kuwa uongozi wa juu upo katika mjadala wakijadili namna ya kumwadhibu mchezaji huyo ambaye hajaichezea timu yao kwa miezi miwili baada ya kutimkia kwao Zimbabwe bila ruhusa ya klabu.
"Tupo kwenye kikao cha kumjadili Ngoma, amekuja jana kutoka kwao Zimbabwe tunachotaka ni kutuambia nani alimpa ruhusa ya kwenda kwao na kingine tunataka kujua kama anataka kucheza Yanga au kuondoka maana tunashindwa kumuelewa kwa yale anayotufanyia," imesema taarifa hiyo.
Chanzo hicho kimedai pamoja na majeruhi aliyokuwa nayo mchezaji huyo lakini alipaswa kubaki nchini kwa ajili ya kufanyiwa matibabu kama ilivyo kwa wenzake wawili Amissi Tambwe na Thabani Kamusoko, lakini yeye aliamua kuondoka kwa maamuzi yake kana kwamba siyo mwajiriwa wa Yanga.
Tangu msimu uliopita Ngoma, amekuwa akiisumbua Yanga na mchango wake kwenye timu umekuwa mdogo ukilinganisha na ilivyokuwa msimu wake wa kwanza ambapo aliweza kufunga mabao 24, katika michuano yote aliyoichezea timu hiyo na kuifikisha hatua ya makundi ya michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika CAF.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Nitapindua dunia juu chini ili kubaki kama meneja wa Arsenal

Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake. Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal Kazi yake katika timu hiyo iliwekwa utatani wakati alipokataa kudhibitsha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror) Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)

Robert Lewandowski mfungaji bora Bundesliga 2017/2018

Robert Lewandowski amemaliza msimu wa 2017/18 wa Bundesliga akiwa mfungaji bora kwa mara ya 3 kwenye maisha yake ya soka. : • 30 games • 29 goals

Je Barcelona wataweza kuvunja rekodi hizi?

Hadi sasa miamba  ya Catalunya Fc Barcelona haijapoteza mchezo hata mmoja katika ligi kuu nchini Hispania na wanaonekana wanaweza kuweka rekodi ya kuwa timu pekee kumaliza La Liga bila kupoteza, lakini je na haya yafuatayo wataweza? Magoli 121, Jose Mourinho msimu wa 2011/2012 alimaliza La Liga akiwa na mabao 121, hadi sasa Barcelona wana mabao 70 na itawabidi kufunga mabao 51 katika mechi zao 11 zilizobaki ili kuifikia rekodi ya Mourinho. Zamora award, hii ni tuzo ya kipa aliyefungwa mabao machache, Francisco Liano mlinda lango wa zamani wa klabu ya Sporting Gijon anashikilia rekodi ya kufungwa mabao machache zaidi La Liga, mabao 18 (1993/1994). Hadi sasa mlinda lango wa Atletico Madrid Jan Oblak ameruhusu mabao 12 katika lango lake huku golikipa wa Barcelona Marc Andre Stegen akiwa ameruhusu mabao 13 hadi sasa, na anasubiriwa kati ya hawa nani atavunja rekodi ya Liano. Real Sociedad record, Barcelona hawajapoteza katika michezo 32 ya La Liga na wamevunja rekodi ya Pep G...