Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Azam Fc: Sisi ndiyo mabingwa

Azam FC imejiwekea malengo ya kufika fainali ya Kombe la FA (Azam Sports Federation Cup) ikiwemo kulitwaa taji hilo msimu huu ambalo linatetewa na Simba.

Kauli hiyo ameitoa Kocha Msaidizi wa timu hiyo, Idd Nassor Cheche, wakati akizungumzia droo ya michuano hiyo iliyotolewa juzi ikishuhudiwa wakipangwa kuanza na Area C United ya Dodoma, amedai kuwa wameipokea vizuri ratiba hiyo na watajipanga kufanya kweli.
“Sisi malengo yetu ni kufika fainali na tuchukue kombe, kwa hiyo kila mtu tutakayepangiwa naye tunajidhatiti, tunajiandaa vizuri ili tuhakikishe ile dhamira yetu inafikia malengo,” alisema Cheche.

Kocha huyo wa muda mrefu ndani ya Azam FC akianzia majukumu ya kuwa Kocha Mkuu kwenye timu ya vijana (Azam U-20) kabla ya kuteuliwa kuwa Kocha Msaidizi Desemba mwaka jana akiwa chini ya Mromania Aristica Cioaba, alisema kuwa wamejipanga vema msimu huu tofauti na mwaka jana.

“Mwaka huu tumejipanga vizuri zaidi tofauti na mwaka jana na tunaari na wachezaji wanaari na tumepata muda kama hivi wa mazoezi tunafanyia kazi matatizo yetu nafikiri mashabiki waje kwa wingi watusapoti na sisi tutawaonyesha kile ambacho wanastahili kuonyeshwa,” alisema.

Azam FC inayodhaminiwa na maji safi ya Uhai Drinking Water, Benki ya NMB na Tradegents, msimu uliopita iliishia nusu fainali ya michuano hiyo baada ya kupoteza dhidi ya Simba kwa bao 1-0, mchezo ambao timu hiyo ilicheza pungufu kwa takribani dakika 75 kufuatia kiungo wake Salum Abubakar ‘Sure Boy, kuonyeshwa kadi nyekundu iliyolalamikiwa kuwa na utata.

Mchezo huo dhidi ya Area C United, umepangwa kufanyika Uwanja wa Azam Complex kati ya Desemba 20 na 25 mwaka huu.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Nitapindua dunia juu chini ili kubaki kama meneja wa Arsenal

Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake. Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal Kazi yake katika timu hiyo iliwekwa utatani wakati alipokataa kudhibitsha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror) Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)

Robert Lewandowski mfungaji bora Bundesliga 2017/2018

Robert Lewandowski amemaliza msimu wa 2017/18 wa Bundesliga akiwa mfungaji bora kwa mara ya 3 kwenye maisha yake ya soka. : • 30 games • 29 goals

Je Barcelona wataweza kuvunja rekodi hizi?

Hadi sasa miamba  ya Catalunya Fc Barcelona haijapoteza mchezo hata mmoja katika ligi kuu nchini Hispania na wanaonekana wanaweza kuweka rekodi ya kuwa timu pekee kumaliza La Liga bila kupoteza, lakini je na haya yafuatayo wataweza? Magoli 121, Jose Mourinho msimu wa 2011/2012 alimaliza La Liga akiwa na mabao 121, hadi sasa Barcelona wana mabao 70 na itawabidi kufunga mabao 51 katika mechi zao 11 zilizobaki ili kuifikia rekodi ya Mourinho. Zamora award, hii ni tuzo ya kipa aliyefungwa mabao machache, Francisco Liano mlinda lango wa zamani wa klabu ya Sporting Gijon anashikilia rekodi ya kufungwa mabao machache zaidi La Liga, mabao 18 (1993/1994). Hadi sasa mlinda lango wa Atletico Madrid Jan Oblak ameruhusu mabao 12 katika lango lake huku golikipa wa Barcelona Marc Andre Stegen akiwa ameruhusu mabao 13 hadi sasa, na anasubiriwa kati ya hawa nani atavunja rekodi ya Liano. Real Sociedad record, Barcelona hawajapoteza katika michezo 32 ya La Liga na wamevunja rekodi ya Pep G...