Meneja wa Manchester City Pep Guardiola amemwelezea David Silva kama kiungo aliyekamilika baada ya kufunga magoli katika mechi za hivi karibuni.
Mchezaji huyo wa Kimataifa wa Hispania ameweka kimiani katika ushindi mwembamba dhidi ya West Ham United na Manchester United kwenye mechi zilizopita, kadhalika mabao mawili aliyofunga dhidi ya Swansea City Jumatano.
Guardiola amemsifia Silva kufuatia kiwango chake maridadi, akidai kuwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31 sasa ni "mnyama" anapokuwa akiwinda goli mbele ya lango.
"Ana kila kitu, hasa anapokuwa dhidi ya wapinzani wakuu." alikiambia BBC Sport. "Kila mmoja anazungumzia ufundi wake, hakuna shaka katika hilo. Hata kipofu anaweza kuona.
"Lakini huwezi kufikiri ni kiasi gani alivyo mahiri dhidi ya wapinzani. Anaonekana kama mtu wa aina tofauti lakini, wow, ni mnyama katika kipengele cha kushinda mech.
"Mara zote tumekuwa tukizungumzia hilo: 'Unahitaji kufunga magoli, David. Unaweza kufanya hivyo. Unahitaji kufunga magoli ili kushinda mechi. Unaweza kufanya hivyo.' Katika kipindi kilichopita goli dhidi ya West Ham na Old Trafford na dhidi ya Swansea ni muhimu sana."
Silva amehusika kwenye magoli 13 Ligi Kuu Uingereza katika mechi 17 msimu huu - tayari amezidi kile alichofanya 2016-17
Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake. Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal Kazi yake katika timu hiyo iliwekwa utatani wakati alipokataa kudhibitsha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror) Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)
Maoni
Chapisha Maoni