Ruka hadi kwenye maudhui makuu

David Silva ni zaidi ya kiungo

Meneja wa Manchester City Pep Guardiola amemwelezea David Silva kama kiungo aliyekamilika baada ya kufunga magoli katika mechi za hivi karibuni.
Mchezaji huyo wa Kimataifa wa Hispania ameweka kimiani katika ushindi mwembamba dhidi ya West Ham United na Manchester United kwenye mechi zilizopita, kadhalika mabao mawili aliyofunga dhidi ya Swansea City Jumatano.
Guardiola amemsifia Silva kufuatia kiwango chake maridadi, akidai kuwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31 sasa ni "mnyama" anapokuwa akiwinda goli mbele ya lango.
"Ana kila kitu, hasa anapokuwa dhidi ya wapinzani wakuu." alikiambia BBC Sport. "Kila mmoja anazungumzia ufundi wake, hakuna shaka katika hilo. Hata kipofu anaweza kuona.
"Lakini huwezi kufikiri ni kiasi gani alivyo mahiri dhidi ya wapinzani. Anaonekana kama mtu wa aina tofauti lakini, wow, ni mnyama katika kipengele cha kushinda mech.
"Mara zote tumekuwa tukizungumzia hilo: 'Unahitaji kufunga magoli, David. Unaweza kufanya hivyo. Unahitaji kufunga magoli ili kushinda mechi. Unaweza kufanya hivyo.' Katika kipindi kilichopita goli dhidi ya West Ham na Old Trafford na dhidi ya Swansea ni muhimu sana."
Silva amehusika kwenye magoli 13 Ligi Kuu Uingereza katika mechi 17 msimu huu - tayari amezidi kile alichofanya 2016-17

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Nitapindua dunia juu chini ili kubaki kama meneja wa Arsenal

Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake. Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal Kazi yake katika timu hiyo iliwekwa utatani wakati alipokataa kudhibitsha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror) Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)

Robert Lewandowski mfungaji bora Bundesliga 2017/2018

Robert Lewandowski amemaliza msimu wa 2017/18 wa Bundesliga akiwa mfungaji bora kwa mara ya 3 kwenye maisha yake ya soka. : • 30 games • 29 goals

Je Barcelona wataweza kuvunja rekodi hizi?

Hadi sasa miamba  ya Catalunya Fc Barcelona haijapoteza mchezo hata mmoja katika ligi kuu nchini Hispania na wanaonekana wanaweza kuweka rekodi ya kuwa timu pekee kumaliza La Liga bila kupoteza, lakini je na haya yafuatayo wataweza? Magoli 121, Jose Mourinho msimu wa 2011/2012 alimaliza La Liga akiwa na mabao 121, hadi sasa Barcelona wana mabao 70 na itawabidi kufunga mabao 51 katika mechi zao 11 zilizobaki ili kuifikia rekodi ya Mourinho. Zamora award, hii ni tuzo ya kipa aliyefungwa mabao machache, Francisco Liano mlinda lango wa zamani wa klabu ya Sporting Gijon anashikilia rekodi ya kufungwa mabao machache zaidi La Liga, mabao 18 (1993/1994). Hadi sasa mlinda lango wa Atletico Madrid Jan Oblak ameruhusu mabao 12 katika lango lake huku golikipa wa Barcelona Marc Andre Stegen akiwa ameruhusu mabao 13 hadi sasa, na anasubiriwa kati ya hawa nani atavunja rekodi ya Liano. Real Sociedad record, Barcelona hawajapoteza katika michezo 32 ya La Liga na wamevunja rekodi ya Pep G...