Kocha wa Barcelona Ernesto Valverde amesema kuwa Ousmane Dembele hatacheza mechi ya Clasico wikiendi ijayo licha ya kuanza mazoezi
Dembele hajacheza tangu alipopata majeraha dhidi ya Getafe Septemba, na kulazimika kukaa nje kwa miezi. Hata hivyo, mshambuliaji huyo wa Kifaransa amerejea kwenye ratiba ya mazoezi, na kuamsha tetesi kuwa anaweza kuwemo kwenye safari ya kwenda Real Madrid Desemba 23.
Lakini Valverde amesema Dembele hatarejea kibaruani hadi Januari, akisisitza kuwa hakuna haja ya kumuingiza mchezaji huyo matatizoni.
"Amefanya mengi kwenye mazoezi wiki hii, lakini hajakamilisha mazoezi kamili hadi sasa," kocha aliwaambia waandishi Jumamosi.
"Wiki ijayo tutamwongezea kazi, lakini mpango ni ule ule wa awali. Januari ndio tunamtarajia kurudi dimbani.
"Itakuwa mapema - na tutamweka matatizoni kumchezesha mapema. Malengo yetu ni kumwacha kwanza hadi Januari."
Kabla ya safari kwenda Bernabeu kwa mechi ya kwanza ya Clasico kwa msimu huu, wataikaribisha Deportivo La Coruna kwenye uwanja wa Camp Nou, na Andres Iniesta na Javier Mascherano watarudi mchezoni Jumapili.
Nahodha Iniesta alikosa mechi mbili za mwisho za Barca kwa sababu ya tatizo la misuli lakini amepona na yupo tayari kwa mechi ya wikiendi hii, wakati Mascherano hajacheza tangu katikati ya mwezi Novemba alipopata majeraha kwenye majukumu ya ktaifa Argentin
Maoni
Chapisha Maoni