Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Eric Baily nje miezi mitatu

Beki wa Manchester United Eric Bailly atafanyiwa upasuajiwa kifundo cha mguu na kukaa nje miezi mitatu
Bosi wa United Jose Mourinho alisema katikati ya juma kuwa beki huyo wa kati atapigwa kisu kurekebisha tatizolae, na amethibitisha Ijumaa kuwa hofu yake imedhihiri.

"Anakwenda kufanyiwa upasuaji, uamuzi umefanyika," Mourinho alisema. "Sisemi kwamba yupo nje kwa muda wote wa msimu, lakini kwa miezi mitatu ijayo."
Mchezaji wa kimataifa wa Ivory Coast Bailly amekosa mechi nane mfululizo, na mechi ya karibuni aliyocheza ni ile waliyofungwa 1-0 na Chelsea November 5
.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 alipata majeraha kwenye majukumu ya kimataifa lakini Mourinho alisema mapema juma hili kuwa anaridhishwa na wanaoweza kuziba pengo lake.

Alisema: "Nimemchezesha [Chris] Smalling na [Phil] Jones na tunaye [Victor] Lindelof na [Daley] Blind kwenye benchi. Marcos Rojo alipata majeraha [dhidi ya Manchester City] lakini tatizo si kubwa.

"Katika msimu wote, tumekuwa na tatizo la mabeki wa kati, lakini kwa sababu namba ni nne au tano, mara zote tunaweza kutumia wachezaji tulio nao.
"Chris Smalling anacheza vizuri sana kwa mechi saba au nane mfululizo, kwa hiyo tuko vizuri."

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Nitapindua dunia juu chini ili kubaki kama meneja wa Arsenal

Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake. Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal Kazi yake katika timu hiyo iliwekwa utatani wakati alipokataa kudhibitsha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror) Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)

Robert Lewandowski mfungaji bora Bundesliga 2017/2018

Robert Lewandowski amemaliza msimu wa 2017/18 wa Bundesliga akiwa mfungaji bora kwa mara ya 3 kwenye maisha yake ya soka. : • 30 games • 29 goals

Je Barcelona wataweza kuvunja rekodi hizi?

Hadi sasa miamba  ya Catalunya Fc Barcelona haijapoteza mchezo hata mmoja katika ligi kuu nchini Hispania na wanaonekana wanaweza kuweka rekodi ya kuwa timu pekee kumaliza La Liga bila kupoteza, lakini je na haya yafuatayo wataweza? Magoli 121, Jose Mourinho msimu wa 2011/2012 alimaliza La Liga akiwa na mabao 121, hadi sasa Barcelona wana mabao 70 na itawabidi kufunga mabao 51 katika mechi zao 11 zilizobaki ili kuifikia rekodi ya Mourinho. Zamora award, hii ni tuzo ya kipa aliyefungwa mabao machache, Francisco Liano mlinda lango wa zamani wa klabu ya Sporting Gijon anashikilia rekodi ya kufungwa mabao machache zaidi La Liga, mabao 18 (1993/1994). Hadi sasa mlinda lango wa Atletico Madrid Jan Oblak ameruhusu mabao 12 katika lango lake huku golikipa wa Barcelona Marc Andre Stegen akiwa ameruhusu mabao 13 hadi sasa, na anasubiriwa kati ya hawa nani atavunja rekodi ya Liano. Real Sociedad record, Barcelona hawajapoteza katika michezo 32 ya La Liga na wamevunja rekodi ya Pep G...