Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Manchester City wailaza Tottenham 4-1

Magoli kutoka kwa Ilkay Gundogan, Kevin De Bruyne na mawili kutoka kwa Raheem Sterling yaliipatia Man City ushindi wa 4-1 dhidi ya Tottenham
Gundogan alifunga goli la kwanza kwa kichwa akiunganisha kona ya Leroy Sane dakika 14 baada ya wenyeji kuumiliki mpira dhidi ya Spurs na waliendelea kutawala mchezo.

Shuti la De Bruyne liliwavunja nguvu Spurs baada ya mpira kuzama wavuni na Sterling aliweka kimiani mara mbili kwa shuti la karibu baada ya kukosa goli la wazi kufuatia Gabriel Jesus kukosa penalti ambayo iligonga mwamba.
Chrstian Eriksen aliipatia Spurs goli la kufutia machozi dakika za mwisho lakini pengo lao dhidi ya vinara hao wa ligi limeongezeka hadi pointi 21.

City wameshawafunga mahasimu wao wote wa taji Ligi Kuu Uingereza msimu huu na mbio zao kuelekea ubingwa wa Uingereza zinaonekana kukosa mpizani.
Walifunga goli lao la kwanza kupitia nafasi yao ya pili, Baada ya Gundogan kuwahadaa mabeki wa Spurs na waliruhusu goli kirahisi mno kupitia Raheem Sterling aliyetupia goli la tatu.

Ukungu ulishuka kwenye uwanja wa Etihad lakini haukuweza kuwazuia City kufanya mambo yao na Hugo Lloris alilazimika kulinda lango hadi kwenda mapumziko wakiwa wa wamefungwa 1-0 tu, Kipa huyo wa Kifaransa aliokoa mara mbili kumzuia Gundogan kufunga goli la pili.

Harry Kane alipiga shuti bomba ambalo lili gonga mwamba Spurs walipotishia kufunga kwa mashambulizi ya kushtukiza, na Mshambuliaji huyo wa Uingereza alikaribia kufunga goli la kusawazisha alipomlazimu Ederson kujinyoosha kuokoa baada ya mapumziko.

Spurs waliongeza nguvu yao lakini mashambulizi ya kushtukiza yaliwagharimu pale De Bruyne alipoweka kimiani dakika ya 70.

Jan Vertonghen alimwangusha De Bruyne ndani ya boksi kwa penalti iliyokuwa dhahiri, lakini Jesus aliyeingia kutokea benchi alipiga mwamba kabla ya Sterling kujaribu kumalizia na kushindwa kwani mpira ulipaa juu.

Sterling alifuta makosa yake ya kukosa magoli ya wazi akiweka kimiani goli rahisi dakika ya 80, kabla ya kufunga jingine kwa kutumia makosa ya Eric Dier baada ya kumpiga tobo Lloris kuipatia City goli la nne.

Spurs wamefanywa zilichofanywa timu nyingine zote zilizotembelea Etihad msimu huu,na Eriksen hakushangilia alipofunga goli la kufutia machozi kwa Spurs dakika za mwisho.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Nitapindua dunia juu chini ili kubaki kama meneja wa Arsenal

Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake. Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal Kazi yake katika timu hiyo iliwekwa utatani wakati alipokataa kudhibitsha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror) Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)

Robert Lewandowski mfungaji bora Bundesliga 2017/2018

Robert Lewandowski amemaliza msimu wa 2017/18 wa Bundesliga akiwa mfungaji bora kwa mara ya 3 kwenye maisha yake ya soka. : • 30 games • 29 goals

Je Barcelona wataweza kuvunja rekodi hizi?

Hadi sasa miamba  ya Catalunya Fc Barcelona haijapoteza mchezo hata mmoja katika ligi kuu nchini Hispania na wanaonekana wanaweza kuweka rekodi ya kuwa timu pekee kumaliza La Liga bila kupoteza, lakini je na haya yafuatayo wataweza? Magoli 121, Jose Mourinho msimu wa 2011/2012 alimaliza La Liga akiwa na mabao 121, hadi sasa Barcelona wana mabao 70 na itawabidi kufunga mabao 51 katika mechi zao 11 zilizobaki ili kuifikia rekodi ya Mourinho. Zamora award, hii ni tuzo ya kipa aliyefungwa mabao machache, Francisco Liano mlinda lango wa zamani wa klabu ya Sporting Gijon anashikilia rekodi ya kufungwa mabao machache zaidi La Liga, mabao 18 (1993/1994). Hadi sasa mlinda lango wa Atletico Madrid Jan Oblak ameruhusu mabao 12 katika lango lake huku golikipa wa Barcelona Marc Andre Stegen akiwa ameruhusu mabao 13 hadi sasa, na anasubiriwa kati ya hawa nani atavunja rekodi ya Liano. Real Sociedad record, Barcelona hawajapoteza katika michezo 32 ya La Liga na wamevunja rekodi ya Pep G...