Njia itakuwa nyeupe kwa Barcelona kumsajili Antoine Griezmann kwa kitita cha paundi £89 milioni kwani Manchester United hawatafanya mchakato wa kumsajili mshambuliaji huyo wa Atletico Madrid kwa mujibu wa Marca .
Barcelona bado inataka kumsajili Angel Di Maria, na Paris Saint-Germain imetaja bei yake kuwa £45 milioni kwa mujibu wa ESPN .Mwargentina huyo si mchezaji muhimu sana kwa PSG tangu ujio wa Neymar na Kylian Mbappe.
Tottenham wamedhamiria kusambaratisha bajeti yao ili kuweza kumbakisha Harry Kane kwenye klabu yao, kwa mujibu wa Daily Mail .
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24, amekuwa kinara wa mabao 2017 akifunga magoli 56, kwa sasa analipwa £110,000 kwa wiki kiasi ambacho ni kidogo kwa wachezaji wa kaliba yake.
Mshahara wa Kane utakuwa unaongezeka kwa mara ya nne tangu Agosti 2014, Spurs wakilenga kuzipindua ofa za Real Madrid.
Klabu za Uingereza zimepata fununu kuwa huenda meneja wa Atletico Madrid Diego Simeone anaweza kumruhusu kuondoka winga wake Yannick Carrasco, kwa mujibu wa AS .
Manchester United na Chelsea zimetajwa kwenye tetesi za kutaka kumsajili Mbelgiji huyo miezi ya hivi karibuni, Mkataba wa Carrasco una thamani ya £86 milioni.
Maoni
Chapisha Maoni