Bosi wa Arsenal, Arsene Wenger amesisitiza kuwa Manchester United hawajawasiliana na Gunners kuhusu uhamisho wa Mesut Ozil.
Kiungo huyo akiwa amebakiwana miezi sita tu kwenye mkataba wake, klabu kadhaa ikiwa ni pamoja na United zimehusishwa na tetesi za kutaka kumsajili Mjerumani huyo.
Hata hivyo, akidai kuwa hana uhakika kuhusu maendeleo ya mazungumzo na Ozil, Wenger amesisitiza kuwa kiungo huyo hataondoka London Kaskazini kabla ya mwisho wa msimu.
Mfaransa huyo aliwaambia waandishi: "Karibu kiasi gani? Sijui ni karibu kiasi gani. Man United hawajawahi kutupigia, kwa hiyo sijui jambo hilo limekujaje.
"Hilo ni jambo ambalo limezushwa. [Atabaki] hadi mwisho wa msimu, mengine yapo wazi."
Pamoja na kuwa Ozil amefunga magoli mawili na sare tano katika mechi 14 Ligi Kuu Uingereza msimu huu, hajafanikiwa kufunga katika mechi tatu za mwisho.
Maoni
Chapisha Maoni