Ulidhani ni rahisi au ni bure kwa Alexis Sanchez kwenda Manchester United? Usijidanganye siyo bure hata kidogo, bali Manchester United watachomoka kiasi kikubwa sana cha pesa kwa mshambuliaji huyo.
£180m United wataitumia katika dili la Sanchez na katika pesa hiyo kiasi cha £35m kinatajwa kama kiasi ambacho Arsenal watavuna endapo watakubali kumuuza Alexis Sanchez kwenda Manchester United.
Kuna pesa nyingine ndefu sana ambayo ni £117m, kiasi hicho cha pesa United watatumia kumlipa mshahara Sanchez wakati wote atakapokuwa katika klabu hiyo na inatajwa kwamba mkataba wake atasaini miaka minne na nusu.
Halafu kuna £20m hii inatajwa ni pesa ambayo Sanchez anaweza kuipata toka United kama akimwaga wino kuitumikia klabu hiyo na usisahau kwamba wakala wake naye atapewa kiasi cha £10m.
Inatajwa kwamba United hawajali hata kidogo kuhusu pesa na wako tayari kutumia pesa yote hiyo kwa Alexis Sanchez ilimradi tu Sanchez asaini katika timu yao, usajili wa Sanchez unaonekana kukwama kwama na bado hakuna taarifa ya uhakika lini atasaini.
Maoni
Chapisha Maoni