Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Atletico Madrid kufungua mashtaka dhidi ya Fc Barcelona

Atletico Madrid wanajiandaa kufungua kesi rasmi FIFA kuhusu suala la Barcelona kuanza mazungumzo kinyume na sheria na mchezaji wao Antonie Griezmann.

Mapema wiki hii iliripotiwa kwenye vyombo vya habari za Hispania kwamba Rais wa Barcelona Josep Maria Bartomeu hivi karibuni alikutana na wazazi wa Griezmann na kuongelea uhamisho wa mchezaji huyo kwenda Nou Camp.

Na kwa mujibu wa taarifa kutoka mtandaonwa AS, Atletico Madrid watairipoti Barcelona kwa mchezo wao mchafu wanaofanya kumsaini mshambuliaji huyo wa Ufaransa.
Atletico wanalalamika kwamba wanaondoa uaminifu kwenye masuala ya uhamisho kwa kujaribu kumsaini Griezmann kinyume na sheria kutoka wapinzani wao wa ligi.

Barca wanaongoza ligi, huku Atletico wakiwa nyuma yao kwa pointi 6 kwenye nafasi ya pili.
Uamuzi wa kuishtaki Barcelona ulifikiwa katika kikao cha wawekezaji mnamo Jumatatu iliyopita, japokuwa kuna urafiki mkubwa kati ya CEO Gil Marin na Rais wa Barca Josep Bartomeu.

Griezmann amekuwa akihusishwa sana na uhamisho wa kuhama Atletico kwenda Barcelona au Manchester United.
Lakini Barcelona wapo kwenye nafasi nzuri zaidi ya kumsaini Antonie na kwa mujibu wa Radio Onda Cero waliripoti wiki hii kwamba dili la uhamisho baina ya mchezaji na klabu hiyo ya Catalunya limeshafikia tamati.

Wakati huo huo, mkurugenzi wa michezo na mahusiano wa Barcelonal Guillermo Amor, jumatatu iliyopita alizungumza maneno yaliyotoa ishara kwamba kuna ukweli juu ya taarifa za uhamisho wa Griezmann kuelekea kukamilika.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Nitapindua dunia juu chini ili kubaki kama meneja wa Arsenal

Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake. Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal Kazi yake katika timu hiyo iliwekwa utatani wakati alipokataa kudhibitsha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror) Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)

Robert Lewandowski mfungaji bora Bundesliga 2017/2018

Robert Lewandowski amemaliza msimu wa 2017/18 wa Bundesliga akiwa mfungaji bora kwa mara ya 3 kwenye maisha yake ya soka. : • 30 games • 29 goals

Je Barcelona wataweza kuvunja rekodi hizi?

Hadi sasa miamba  ya Catalunya Fc Barcelona haijapoteza mchezo hata mmoja katika ligi kuu nchini Hispania na wanaonekana wanaweza kuweka rekodi ya kuwa timu pekee kumaliza La Liga bila kupoteza, lakini je na haya yafuatayo wataweza? Magoli 121, Jose Mourinho msimu wa 2011/2012 alimaliza La Liga akiwa na mabao 121, hadi sasa Barcelona wana mabao 70 na itawabidi kufunga mabao 51 katika mechi zao 11 zilizobaki ili kuifikia rekodi ya Mourinho. Zamora award, hii ni tuzo ya kipa aliyefungwa mabao machache, Francisco Liano mlinda lango wa zamani wa klabu ya Sporting Gijon anashikilia rekodi ya kufungwa mabao machache zaidi La Liga, mabao 18 (1993/1994). Hadi sasa mlinda lango wa Atletico Madrid Jan Oblak ameruhusu mabao 12 katika lango lake huku golikipa wa Barcelona Marc Andre Stegen akiwa ameruhusu mabao 13 hadi sasa, na anasubiriwa kati ya hawa nani atavunja rekodi ya Liano. Real Sociedad record, Barcelona hawajapoteza katika michezo 32 ya La Liga na wamevunja rekodi ya Pep G...