Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Conte: Chielin wa nini?

Kocha mkuu wa Chelsea Antonio Conte amefutilia mbali madai kuwa ana mpango wa kumsajili beki wa Juventus Giorgio Chiellini

Conte yupo sokoni kwa ajili ya kutafuta wachezaji wachache katika dirisha la uhamisho wa Januari na David Luiz amekuwa akihusishwa na tetesi za kuwa mbioni kuondoka Stamford Bridge, Chiellini akitajwa kuwa miongoni mwa wanaweza kuirithi nafasi yake.

Hata hivyo, licha ya kuwahi kufanya kazi na Muitaliano huyo hapo awali, Conte anasema kuwa hajafikiria kumleta Chiellini Premier League.
Kocha huyo mwenye umri wa miaka 48 sasa aliwaambia waandishi: "Kwenye soko la uhamisho kuna tetesi. Sisi tutafanya kilicho chema kwa ajili ya timu.

"Ni lazima niwe mkweli. Giorgio ni mchezaji shupavu na bora lakini anataka kumalizia soka lake Juventus. Ni sahihi kumaliza soka kwa namna hii."

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 33 amedumu Turin kwa muda wa miaka 12 na nusu, akicheza jumla ya mechi 453 katika michuano yote.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Nitapindua dunia juu chini ili kubaki kama meneja wa Arsenal

Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake. Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal Kazi yake katika timu hiyo iliwekwa utatani wakati alipokataa kudhibitsha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror) Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)

Robert Lewandowski mfungaji bora Bundesliga 2017/2018

Robert Lewandowski amemaliza msimu wa 2017/18 wa Bundesliga akiwa mfungaji bora kwa mara ya 3 kwenye maisha yake ya soka. : • 30 games • 29 goals

Je Barcelona wataweza kuvunja rekodi hizi?

Hadi sasa miamba  ya Catalunya Fc Barcelona haijapoteza mchezo hata mmoja katika ligi kuu nchini Hispania na wanaonekana wanaweza kuweka rekodi ya kuwa timu pekee kumaliza La Liga bila kupoteza, lakini je na haya yafuatayo wataweza? Magoli 121, Jose Mourinho msimu wa 2011/2012 alimaliza La Liga akiwa na mabao 121, hadi sasa Barcelona wana mabao 70 na itawabidi kufunga mabao 51 katika mechi zao 11 zilizobaki ili kuifikia rekodi ya Mourinho. Zamora award, hii ni tuzo ya kipa aliyefungwa mabao machache, Francisco Liano mlinda lango wa zamani wa klabu ya Sporting Gijon anashikilia rekodi ya kufungwa mabao machache zaidi La Liga, mabao 18 (1993/1994). Hadi sasa mlinda lango wa Atletico Madrid Jan Oblak ameruhusu mabao 12 katika lango lake huku golikipa wa Barcelona Marc Andre Stegen akiwa ameruhusu mabao 13 hadi sasa, na anasubiriwa kati ya hawa nani atavunja rekodi ya Liano. Real Sociedad record, Barcelona hawajapoteza katika michezo 32 ya La Liga na wamevunja rekodi ya Pep G...