Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Dembele kurejea dimbani.

Mchezaji aliyenunuliwa pesa nyingi zaidi na Barcelona Ousmane Dembele huenda akarejea kucheza wiki hii baada ya kukaa nje ya uwanja wa karibu miezi minne.

Mshambuliaji huyo wa Ufaransa mwenye miaka 20 alijiunga na Barca Agosti kwa £96.8m lakini akaumia akichezea klabu hiyo mechi yake ya tatu - dhidi ya Getafe mnamo 16 Septemba.
Dembele alifanyiwa upasuaji nchini Finland.
Sasa, huenda akarejea kucheza dhidi ya Celta Vigo katika Copa del Rey Alhamisi.

Viongozi wa ligi Barcelona kisha watakutana na Levante katika La Liga Jumapili.
Barca ambao wamo alama tisa mbele kileleni kwenye ligi wamepangiwa kukutana na Chelsea hatua ya 16 bora Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya Februari na Machi.

Dembele - aliyejiunga nao kutoka Borussia Dortmund - ndiye mchezaji wa pili ghali zaidi duniani ba bei yake ya uhamisho inaweza kupanda hadi £135.5m.
Pesa walizolipa Barcelona mwanzoni zilikuwa karibu nusu ya £200m walizopokea kutoka Paris St-Germain kwa mshambuliaji Mbrazil Neymar.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Nitapindua dunia juu chini ili kubaki kama meneja wa Arsenal

Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake. Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal Kazi yake katika timu hiyo iliwekwa utatani wakati alipokataa kudhibitsha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror) Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)

Robert Lewandowski mfungaji bora Bundesliga 2017/2018

Robert Lewandowski amemaliza msimu wa 2017/18 wa Bundesliga akiwa mfungaji bora kwa mara ya 3 kwenye maisha yake ya soka. : • 30 games • 29 goals

Je Barcelona wataweza kuvunja rekodi hizi?

Hadi sasa miamba  ya Catalunya Fc Barcelona haijapoteza mchezo hata mmoja katika ligi kuu nchini Hispania na wanaonekana wanaweza kuweka rekodi ya kuwa timu pekee kumaliza La Liga bila kupoteza, lakini je na haya yafuatayo wataweza? Magoli 121, Jose Mourinho msimu wa 2011/2012 alimaliza La Liga akiwa na mabao 121, hadi sasa Barcelona wana mabao 70 na itawabidi kufunga mabao 51 katika mechi zao 11 zilizobaki ili kuifikia rekodi ya Mourinho. Zamora award, hii ni tuzo ya kipa aliyefungwa mabao machache, Francisco Liano mlinda lango wa zamani wa klabu ya Sporting Gijon anashikilia rekodi ya kufungwa mabao machache zaidi La Liga, mabao 18 (1993/1994). Hadi sasa mlinda lango wa Atletico Madrid Jan Oblak ameruhusu mabao 12 katika lango lake huku golikipa wa Barcelona Marc Andre Stegen akiwa ameruhusu mabao 13 hadi sasa, na anasubiriwa kati ya hawa nani atavunja rekodi ya Liano. Real Sociedad record, Barcelona hawajapoteza katika michezo 32 ya La Liga na wamevunja rekodi ya Pep G...