Pep Guardiola anatarajia Alexis Sanchez atabaki Arsenal Januari licha ya kocha huyo wa Manchester City kubashiri kuwa Gabriel Jesus atakuwa nje kwa muda usiopungua miezi miwili.
Nyota huyo wa kimataifa wa Chile, ambaye anaingia kwenye miezi sita ya mwisho kwenye mkataba wake, alihusishwa na tetesi za kutua City mwanzo wa msimu na alikuwa karibu kuondoka Emirates kabla ya dirisha la usajili kufungwa.
Na baada ya Jesus kupata majeraha, Guardiola anatarajia Mbrazili huyo atakuwa nje ya dimba kwa muda wa takribani miezi mwili baada ya sare ya 0-0 dhidi ya Crystal Palace, Bosi huyo wa zamani wa Barcelona aliukuzwa kama habari hizo zinaweza kumlazimu kumsajili mara moja mchezaji huyo wa zamani wa Barcelona.
Lakini Guardiola hadhani kama Sanchez ataondoka Arsenal ndani ya wiki chache zijazo.
"Sijui," aliwaambia waandishi alipoulizwa ikiwa Sanchez atakuwa kwenye nafasi nzuri kutua City.
"Ni mchezaji wa Arsenal na nadhani ataendelea kubaki pale. Tutakuwa na mkutano wa ndani na tutaona kipi chema [kwa maana ya uhamisho] , lakini yeye ni mchezaji wa Arsenal na nadhani [atabaki]."
Maoni
Chapisha Maoni