Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Kumbe Van Dijk alikuwa muosha sufuria

Safari ya mafanikio mara zote huwa ni ngumu sana, huwa sio rahisi kufikia kilele cha mafanikio kirahisi rahisi na hii ndio imemtokea pia mlinzi mpya wa Liverpool aliyenunuliwa toka Southamoton Virgil Van Djik.

Djik kwa sasa amekuwa habari kubwa ya dunia baada ya rekodi ya usajili aliyoweka, kwa sasa Van Djik ndio mlinzi ghali duniani akinunuliwa kwa £75m huku kwa mwaka akiweka kwenye account kiasi cha £10m.

Akiwa kijana mdogo wa miaka 16 Djik alikuwa hana kitu mfukoni na ilimfanya Djik kutafuta kazi ili kujiendeleza kimaisha na ndipo hapo aliamua kufanya kazi ya kuosha vyombo nchini kwao Uholanzi.

Katika mji anaotokea wa Brenda alifanya kazi hii kwa ujira mdogo sana huku wafanyakazi wenzake wakimuambia asahau kuhusu soka ni ngumu kutoka akiwa huko bali aendelee na kazi ya kuosha masufuria.

Djik hakutaka kusikia la mtu kwani aliamini soka ndio kitu chake cha kumtoa na sasa hadi mmiliki wa mgahawa ambao Djik alikuwa akifanyia kazi haamini kwamba mfanyakazi wake wa zamani amenunuliwa kiasi hicho.
Jacques Lips ambaye ni mmiliki wa mgahawa aliokiwa akifanya kazi Djik amesema aliposikia kiasi hicho cha pesa ilimbidi kurudia mara mbili mbili kutaja pesa hiyo kwani ni kiasi kikubwa mnoo cha pesa.

Jacques Lips akimuongelea Djik anasema “alikuwa anafanya kazi sana na pia alionekana kupenda sana mchezo wa soka, wakati mwingine nilimuambia achana na mambo yako ya soka endelea kuosha vyombo”.

Mmiliki huyo wa mgahawa anasema hawawezi kumsahau Djik kwani alikuwa mtu poa sana na hata namba yake ya simu ameiandika kwenye kitabu cha wafanyakazi na atampigia kumpa hongera.

Pamoja na mafanikio makubwa ambayo Djik ameyapata lakini mlinzi huyo hajasahau mji wao wa Breda na huwa anarudi kwenda kuwasalimia na kutoa shukurani kwa makocha na timu zilizomfungulia njia.

Kabla ya kutua Liverpool , Djik alicheza mtaani kwao Breda, kisha akajiunga na Willem ii baadaye akaenda FC Groningen zote za Uholanzi, kisha akanunuliwa Celtic waliomuuza Southampton na sasa Liverpool.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Nitapindua dunia juu chini ili kubaki kama meneja wa Arsenal

Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake. Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal Kazi yake katika timu hiyo iliwekwa utatani wakati alipokataa kudhibitsha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror) Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)

Robert Lewandowski mfungaji bora Bundesliga 2017/2018

Robert Lewandowski amemaliza msimu wa 2017/18 wa Bundesliga akiwa mfungaji bora kwa mara ya 3 kwenye maisha yake ya soka. : • 30 games • 29 goals

Je Barcelona wataweza kuvunja rekodi hizi?

Hadi sasa miamba  ya Catalunya Fc Barcelona haijapoteza mchezo hata mmoja katika ligi kuu nchini Hispania na wanaonekana wanaweza kuweka rekodi ya kuwa timu pekee kumaliza La Liga bila kupoteza, lakini je na haya yafuatayo wataweza? Magoli 121, Jose Mourinho msimu wa 2011/2012 alimaliza La Liga akiwa na mabao 121, hadi sasa Barcelona wana mabao 70 na itawabidi kufunga mabao 51 katika mechi zao 11 zilizobaki ili kuifikia rekodi ya Mourinho. Zamora award, hii ni tuzo ya kipa aliyefungwa mabao machache, Francisco Liano mlinda lango wa zamani wa klabu ya Sporting Gijon anashikilia rekodi ya kufungwa mabao machache zaidi La Liga, mabao 18 (1993/1994). Hadi sasa mlinda lango wa Atletico Madrid Jan Oblak ameruhusu mabao 12 katika lango lake huku golikipa wa Barcelona Marc Andre Stegen akiwa ameruhusu mabao 13 hadi sasa, na anasubiriwa kati ya hawa nani atavunja rekodi ya Liano. Real Sociedad record, Barcelona hawajapoteza katika michezo 32 ya La Liga na wamevunja rekodi ya Pep G...