Siku hizi kila mahali pesa ndio kila kitu, mwenye pesa anaweza kugeuza kila kitu ndani ya muda mfupi. Hivyo ndio unavyoweza kusema baada ya Florentino Perez kuamua kutangaza vita kubwa sokoni.
Madrid wanaonekana kuyumba sana msimu huu na hakuna matumaini ya kombe lolote huku wapinzani wao Barcelona wakiwa katika msimu bora kuanzia uwanjani na hadi sokoni katika soko hili la usajili.
Sasa Madrid wameamua kujiandaa kulipa kisasi katika manunuzi na kiasi cha £500m kimetengwa kwa ajili ya kufanya usajili wa nyota watatu wakubwa katika dirisha kubwa lijalo la usajili.
£500m yote inaonekana kuelekezwa katika ligi kuu ha Uingereza EPL na kwanza wataanza na Manchester United ambapo watamwaga £100m kwa ajili ya kumsajili golikipa wa Manchester United David De Gea anayetajwa kuwa na thamani zaidi ya £75m.
Madrid hawaishii hapo wanataka kuivamia tena Tottenham Hotspur na wanaamini kiasi cha £200m kinaweza kuwashawishi Tottenham kumuuza mchezaji wao bora kinara wa mabao EPL Harry Kane.
Lakini £200m iliyobaki Madrid watarudi tena Chelsea kuwashawishi kumuuza Eden Hazard ambaye inadaiwa kwamba sio tu kwamba ni kipenzi cha Zinedine Zidane bali hata Florentino Perez anamhusudu Mbelgiji huyo.
Maoni
Chapisha Maoni