Jose Mourinho amesema hawezi kumzuia Zlatan Ibrahimovic endapo atataka kuondoka Manchester United ikiwa mshambuliaji wa Kiswiden ataaonyesha hamu ya kuondoka.
Pamoja na kuwepo kwa fununu kuwa mchezaji huyo anaweza kwenda La Galaxy, Mourinho amesema "Hakuniambia kitu kuhusu hilo mara ya kwanza nilivyosoma au kusikia kuhusu hilo kilichotokea kutoka kwa waandishi wa habari. Yeye hakuniambia kitu kamwe kuhusu hilo hivyo sijui. "
"Ni mwaka wa mwisho katika mkataba wa Zlatan Ibrahimovic . Ikiwa ni kweli Zlatan anataka kwenda katika klabu nyingine katika nchi nyingine tuko hapa kusaidia na kuunda mazingira kwa ajili hiyo, sio kufanya maisha yake kuwa magumu."
Maoni
Chapisha Maoni