Msimu wa 2005-2006 ulikuwa msimu wa mwisho kwa CR7 kuumaliza akiwa na mabao machache zaidi katika ligi, msimu huo Cristiano Ronaldo alicheza michezo 33 lakini akamaliza akiwa na mabao 9 tu.
Hii leo ni tarehe 15 January 2018 raundi ya pili ya La Liga Cristiano Ronaldo ana mabao 4 tu, tangu ajiunge na Real Madrid hajwahi kufika wakati kama huu akiwa na idadi ndogo ya mabao kiasi hicho.
Msimu wa mwaka 2014/2015 wakati kama huu mwezi wa kwanza tayari CR7 alikuwa ameshacheka na nyavu mara 28 lakini sasa anahangaika na wastani unaonesha anafunga bao moja kila baada ya dakika 311, rekodi mbovu zaidi kwake.
Mbaya zaidi kwa Cr7 hajawahi kuachwa kiasi hichi na mpinzani wake Lioneil Messi kwa idadi ya mabao katika kipindi kama hiki, Messi ana mabao 16 hadi sasa ikiwa ni tofauti ya mabao 12 na alipo CR7.
Lakini hilo ni La Liga tu ila huko kwingineko katika Champions League kama kawaida yake Mreno huyo anaendeleza uswahiba wake na nyavu ambapo michezo yake 6 ana mabao 9, lakini kwa umri wa sasa wa CR7(33) inaweza kuwa ndio mwisho wa CR7? Tusubiri tuone.
Maoni
Chapisha Maoni