Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tetesi za soka Ulaya Alhamisi 4 Januari 2018

Mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez amekubali kwa maneno ya kinywa kujiunga na Manchester City, kwa mujibu wa Marca .
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Chile alikaribia kujiunga na City msimu wa majira ya joto na inaonekana anataka kumaliza mkataba wake ambao utaisha mwisho wa msimu huu Emirates.

Inter wanataamani kumsajili kiungo wa Manchester United Juan Mata, kwa mujibu wa Daily Mirror .
Muhispania huyo atakuwa amemaliza mkataba wake Old Trafford ifikapo mwisho wa msimu huu, ingawa anayo fursa ya kuongeza mkataba wake kwa mwaka mmoja zaidi.

Manchester United wameanza kuhofu kuwa Jose Mourinho anaweza kujiuzulu kazi mwisho wa msimu huu kwa mujibu wa Daily Mail .
Kocha huyo wa zamani wa Chelsea amekuwa katika kipindi kigumu wiki za hivi karibuni baada ya timu yake kujikuta nyuma ya Manchester City kwa pointi 15 katika mbio za ubingwa na ameweka bayana hadharani kuwa United hawajatumia fedha za kutosha kuwa washindani.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Nitapindua dunia juu chini ili kubaki kama meneja wa Arsenal

Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake. Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal Kazi yake katika timu hiyo iliwekwa utatani wakati alipokataa kudhibitsha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror) Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)

Robert Lewandowski mfungaji bora Bundesliga 2017/2018

Robert Lewandowski amemaliza msimu wa 2017/18 wa Bundesliga akiwa mfungaji bora kwa mara ya 3 kwenye maisha yake ya soka. : • 30 games • 29 goals

Je Barcelona wataweza kuvunja rekodi hizi?

Hadi sasa miamba  ya Catalunya Fc Barcelona haijapoteza mchezo hata mmoja katika ligi kuu nchini Hispania na wanaonekana wanaweza kuweka rekodi ya kuwa timu pekee kumaliza La Liga bila kupoteza, lakini je na haya yafuatayo wataweza? Magoli 121, Jose Mourinho msimu wa 2011/2012 alimaliza La Liga akiwa na mabao 121, hadi sasa Barcelona wana mabao 70 na itawabidi kufunga mabao 51 katika mechi zao 11 zilizobaki ili kuifikia rekodi ya Mourinho. Zamora award, hii ni tuzo ya kipa aliyefungwa mabao machache, Francisco Liano mlinda lango wa zamani wa klabu ya Sporting Gijon anashikilia rekodi ya kufungwa mabao machache zaidi La Liga, mabao 18 (1993/1994). Hadi sasa mlinda lango wa Atletico Madrid Jan Oblak ameruhusu mabao 12 katika lango lake huku golikipa wa Barcelona Marc Andre Stegen akiwa ameruhusu mabao 13 hadi sasa, na anasubiriwa kati ya hawa nani atavunja rekodi ya Liano. Real Sociedad record, Barcelona hawajapoteza katika michezo 32 ya La Liga na wamevunja rekodi ya Pep G...