Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tetesi za soka Ulaya Ijumaa 19 Januari 2017

Klabu ya Chelsea inatajwa kuingia rasmi katika vita ya kumnunua mshambuliaji wa As Roma Edin Dzeko ambapo Chelsea wanajipanga kutoa £50m kwa ajili ya mshambuliaji huyo pamoja na mlinzi wa kushoto wa Roma Emerson Palmieri.

Juventus wanaonekana wamerudi katika klabu ya Arsenal na sasa wanataka kumchukua beki wao Hector Bellerin, Juventus wanatajwa kwamba wako tayari kutoa kiasi cha £40m kwa ajili ya kumnunua Bellerin.

Klabu ya Manchester United inatajwa kuanza mazungumzo na golikipa wao David De Gea ili kujaribu kumuongezea mkataba, United wanataka kumpa De Gea mkataba mpya ili kumzuia asiende Real Madrid.

Inadaiwa kwamba klabu ya Tottenham Hotspur imeingia katika vita na Manchester United kwa ajili ya kumsajili winga wa PSG Lucas Moura ambaye anatajwa kwamba siku zake kuitumikia PSG zimekaribia kuisha.

Jean Michael Seri kiungo wa Ivory Coast anatajwa kuwaweka vitani Chelsea, PSG na Manchester City ambapo vilabu vyote hivyo vitatu vinatajwa kuhitaji huduma ya kiungo huyo wa Nice.

Inadaiwa kwamba klabu ya Real Madrid iko mbioni kufanya kufuru katika soko la usajili ambapo wanatajwa kutaka kuwanunua Roberto Lewandoski, Neymar pamoja na Eden Hazard kutoka Chelsea.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Nitapindua dunia juu chini ili kubaki kama meneja wa Arsenal

Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake. Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal Kazi yake katika timu hiyo iliwekwa utatani wakati alipokataa kudhibitsha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror) Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)

Robert Lewandowski mfungaji bora Bundesliga 2017/2018

Robert Lewandowski amemaliza msimu wa 2017/18 wa Bundesliga akiwa mfungaji bora kwa mara ya 3 kwenye maisha yake ya soka. : • 30 games • 29 goals

Je Barcelona wataweza kuvunja rekodi hizi?

Hadi sasa miamba  ya Catalunya Fc Barcelona haijapoteza mchezo hata mmoja katika ligi kuu nchini Hispania na wanaonekana wanaweza kuweka rekodi ya kuwa timu pekee kumaliza La Liga bila kupoteza, lakini je na haya yafuatayo wataweza? Magoli 121, Jose Mourinho msimu wa 2011/2012 alimaliza La Liga akiwa na mabao 121, hadi sasa Barcelona wana mabao 70 na itawabidi kufunga mabao 51 katika mechi zao 11 zilizobaki ili kuifikia rekodi ya Mourinho. Zamora award, hii ni tuzo ya kipa aliyefungwa mabao machache, Francisco Liano mlinda lango wa zamani wa klabu ya Sporting Gijon anashikilia rekodi ya kufungwa mabao machache zaidi La Liga, mabao 18 (1993/1994). Hadi sasa mlinda lango wa Atletico Madrid Jan Oblak ameruhusu mabao 12 katika lango lake huku golikipa wa Barcelona Marc Andre Stegen akiwa ameruhusu mabao 13 hadi sasa, na anasubiriwa kati ya hawa nani atavunja rekodi ya Liano. Real Sociedad record, Barcelona hawajapoteza katika michezo 32 ya La Liga na wamevunja rekodi ya Pep G...