Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tetesi za soka Ulaya Ijumaa 26 Januari 2017

Baada ya Alexis Sanchez kuondoka Arsenal sasa klabu hiyo iko tayari kutuma ofa kwa PSG kwa ajili ya kumnunua Lucas Moura ambaye Arsene Wenger anamuona kama mtu sahihi wa kuvaa viatu vya Sanchez.

Inadaiwa kwamba mshambuliaji wa klabu ya Arsenal Olivier Giroud anaweza kufanya usajili wa mshambuliaji wa Borussia Dortmund Pierre Aubameyang usitokee kwani hana mpango wa kwenda Dortmund.

Kocha wa Real Madrid Zinedine Zidane amekiri kwamba kwa sasa kazi yake haiko mashakani sana lakini amekiri kwamba mechi yao na PSG inaweza kuamua hatma yake ndani ya klabu hiyo ya Real Madrid.

Real Madrid wanataka kurudi tena kwa Manchester United kumuwinda mlinda lango wao David De Gea na taarifa zinasema kwamba tayari Madrid wameshamwambia wakala wa De Gea kuhusu nia yao hiyo.

Pep Gurdiola anatajwa kuingia kwenye vita ya kumnasa Antoine Griezman toka Atletico Madrid na Manchester City wanataka kumtumia Kun Aguero aende Atletico na wao wamchukue Mfaransa huyo.

Klabu ya As Roma imekanusha taarifa kwamba wamekubaliana ada ya uhamisho na Chelsea, wakati huo huo wakala wa Dzeko anadaiwa kushindwa kusafiri kwenda Uingereza kutokana na matatizo ya Visa na hivyo Chelsea itawabidi kusubiri hadi ashughulikie tatizo hilo.

Jose Mourinho anaonekana anataka tena kuingilia uhamisho wa Chelsea na sasa amepanga kuwapa upinzani kumnunua mlinzi wa kushoto wa Juventus Alex Sandro anayetajwa kuwa mrithi wa Luke Shaw.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Nitapindua dunia juu chini ili kubaki kama meneja wa Arsenal

Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake. Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal Kazi yake katika timu hiyo iliwekwa utatani wakati alipokataa kudhibitsha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror) Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)

Robert Lewandowski mfungaji bora Bundesliga 2017/2018

Robert Lewandowski amemaliza msimu wa 2017/18 wa Bundesliga akiwa mfungaji bora kwa mara ya 3 kwenye maisha yake ya soka. : • 30 games • 29 goals

Je Barcelona wataweza kuvunja rekodi hizi?

Hadi sasa miamba  ya Catalunya Fc Barcelona haijapoteza mchezo hata mmoja katika ligi kuu nchini Hispania na wanaonekana wanaweza kuweka rekodi ya kuwa timu pekee kumaliza La Liga bila kupoteza, lakini je na haya yafuatayo wataweza? Magoli 121, Jose Mourinho msimu wa 2011/2012 alimaliza La Liga akiwa na mabao 121, hadi sasa Barcelona wana mabao 70 na itawabidi kufunga mabao 51 katika mechi zao 11 zilizobaki ili kuifikia rekodi ya Mourinho. Zamora award, hii ni tuzo ya kipa aliyefungwa mabao machache, Francisco Liano mlinda lango wa zamani wa klabu ya Sporting Gijon anashikilia rekodi ya kufungwa mabao machache zaidi La Liga, mabao 18 (1993/1994). Hadi sasa mlinda lango wa Atletico Madrid Jan Oblak ameruhusu mabao 12 katika lango lake huku golikipa wa Barcelona Marc Andre Stegen akiwa ameruhusu mabao 13 hadi sasa, na anasubiriwa kati ya hawa nani atavunja rekodi ya Liano. Real Sociedad record, Barcelona hawajapoteza katika michezo 32 ya La Liga na wamevunja rekodi ya Pep G...