Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tetesi za soka Ulaya Ijumaa 5 Januari 2018

Arsenal wataangalia uwezekano wa kumsajili mshambuliaji wa Borussia Dortmund Pierre Emerick Aubameyang ikiwa Alexis Sanchez ataondoka uhamisho wa Januari kwa mujibu wa
Gianluca Di Marzio .
Alexis Sanchez bado yupo kwenye rada za Manchester City kwani mkataba wake unazidi kuelekea ukiongoni Emirates.
Na Gunners wameshaanza kufanya mipango ya kutafuta mbadala wake, Aubameyang akipewa kiapumbele.

Kocha mkuu wa Monaco, Leonardo Jardim amesisitiza kuwa Thomas Lemar hataondoka klabuni hapo uhamisho wa Januari.
Mchezaji huyo amekuwa shabaha ya muda mrefu ya Liverpool na Arsenal, lakini Jardim amesisitiza kuwa Lemar hataondoka Monaco hadi majira ya joto.
"Monaco haina tabia ya kuuza wachezaji majira ya baridi. Ni mkakati wetu. Wachezaji wanaelewa na wanafahamu jinsi mambo yanavyokwenda hapa", alisema Jardim.

Manchester City wapo tayari kutoa kitita cha paundi milioni 35 kwa ajili ya kumsajili mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez kwa mujibu wa DailyMail.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Nitapindua dunia juu chini ili kubaki kama meneja wa Arsenal

Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake. Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal Kazi yake katika timu hiyo iliwekwa utatani wakati alipokataa kudhibitsha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror) Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)

Robert Lewandowski mfungaji bora Bundesliga 2017/2018

Robert Lewandowski amemaliza msimu wa 2017/18 wa Bundesliga akiwa mfungaji bora kwa mara ya 3 kwenye maisha yake ya soka. : • 30 games • 29 goals

Je Barcelona wataweza kuvunja rekodi hizi?

Hadi sasa miamba  ya Catalunya Fc Barcelona haijapoteza mchezo hata mmoja katika ligi kuu nchini Hispania na wanaonekana wanaweza kuweka rekodi ya kuwa timu pekee kumaliza La Liga bila kupoteza, lakini je na haya yafuatayo wataweza? Magoli 121, Jose Mourinho msimu wa 2011/2012 alimaliza La Liga akiwa na mabao 121, hadi sasa Barcelona wana mabao 70 na itawabidi kufunga mabao 51 katika mechi zao 11 zilizobaki ili kuifikia rekodi ya Mourinho. Zamora award, hii ni tuzo ya kipa aliyefungwa mabao machache, Francisco Liano mlinda lango wa zamani wa klabu ya Sporting Gijon anashikilia rekodi ya kufungwa mabao machache zaidi La Liga, mabao 18 (1993/1994). Hadi sasa mlinda lango wa Atletico Madrid Jan Oblak ameruhusu mabao 12 katika lango lake huku golikipa wa Barcelona Marc Andre Stegen akiwa ameruhusu mabao 13 hadi sasa, na anasubiriwa kati ya hawa nani atavunja rekodi ya Liano. Real Sociedad record, Barcelona hawajapoteza katika michezo 32 ya La Liga na wamevunja rekodi ya Pep G...