Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tetesi za soka Ulaya Jumamosi 6 Januari 2018

Mafanikio ya Mohamed Salah mapema msimu huu akiwa Liverpool yameifanya Real Madrid kuvutiwa naye, kwa mujibu wa OK Diario.
Vijana wa Zinedine Zidane wameshindwa kufanya maajabu mbele ya goli na wanatafuta utatuzi wa tatizo hilo, mchezaji huyo wa kimataifa wa Misri anapewa nafasi kubwa kutua Bernabeu.
Madrid wanatambua kuwa kukamilika kwa dili hilo kwa uhamisho wa Januari ni vigumu kwa hiyo wanajipanga kwa ajili ya majira ya joto.

Guangzhou Evergrande wamefikia makubaliano na Pierre-Emerick Aubameyang na Borussia Dortmund ya uhamisho wa mchezaji huyo wa kimataifa wa Gabon majira ya joto, kwa mujibu wa Sima Sports.
Klabu hiyo ya Chinese Super League italazimika kutoa kitita cha €72 milioni kuhakikish mshambuliaji huyo anatua Beijing, wakiwa wameshatoa dau la €60m.

Meneja w Arsenal, Arsene Wenger hajakataa uwezekano wa Alexis Sanchez kuondoka, na ikiwa mchezaji huyo wa Chile ataondoka kwenda Man City Januari, atakuwa tayari kumsajili Thomas Lemar wa Monaco kuwa mrithi wake, kwa mujibu wa L'Equipe .
The Gunners walishindwa kumsajili Lemar majira ya joto kwa kitita cha £90 ingawa meneja wa Monaco Jardim amesisitiza kuwa Mfaransa huyo hauzwi, lakini Wenger anaweza kufanya jaribio la kumsajili ikiwa Sanchez ataondoka..

Philippe Coutinho yupo tayari kutoa €15m kutoka mfukoni mwke binafsi kuwezesha uhaisho wake kutoka Liverpool kwenda Barcelona, kwa mujibu wa Mundo Deportivo .
Nyota huyo wa Kibrazili ameshakataa ofa nono kutoka Real Madrid na Paris Saint-Germain, moyo wake umeeleke Camp Nou.

Manchester City wanajipanga kutoa dau la £35 milioni kwa ajili ya Alexis Sanchez anayetaka kuondoka Arsenal kwa mujibu wa Daily Mail .
Majeraha ya goti ya Gabriel Jesus yamemlazimu Pep Guardiola kufikiria kumsajilimchezaji huyo wa kimataifa wa Chile, ambaye amekuwa akivutiwa naye tangu majira ya joto.

Beki wa kati wa Chelsea David Luiz atatolewa kwa mkopo nusu ya pili ya msimu, kwa mujibu wa The Express .
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Brazili alipishana kauli na meneja Antonio Conte ambaye sasa anataka kumwondoa Darajani beki huyo mzoefu.

Eden Hazard ameikataa ofa ya pili kusaini mkataba mpya Chelsea kwa mujibu wa RMC .
Mchezji huyo wa kimataifa wa Ubelgiji mkataba wake wa sasa unaishia 2020, lakini Blues wanataka kumpa mkataba zaidi kumzuia kwenda Real Madrid.
Inasadikiw kuwa Antonio Conte amekasirishwa na kitendo cha Hazard kukataa kusaini mkataba mpya, ambao ungemfanya Mbelgiji huyo kuwa mchezaji anayepokea mshahara mnono katika historia ya Chelse.
Man Utd yaanza kum

Manchester United wapo tayari kuuvuruga mchakato wa Real Madrid kumsajili mshambuliaji wa Tottenham Harry Kane, kwa mujibu wa Don Balon , via the Manchester Evening News .

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Nitapindua dunia juu chini ili kubaki kama meneja wa Arsenal

Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake. Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal Kazi yake katika timu hiyo iliwekwa utatani wakati alipokataa kudhibitsha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror) Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)

Robert Lewandowski mfungaji bora Bundesliga 2017/2018

Robert Lewandowski amemaliza msimu wa 2017/18 wa Bundesliga akiwa mfungaji bora kwa mara ya 3 kwenye maisha yake ya soka. : • 30 games • 29 goals

Je Barcelona wataweza kuvunja rekodi hizi?

Hadi sasa miamba  ya Catalunya Fc Barcelona haijapoteza mchezo hata mmoja katika ligi kuu nchini Hispania na wanaonekana wanaweza kuweka rekodi ya kuwa timu pekee kumaliza La Liga bila kupoteza, lakini je na haya yafuatayo wataweza? Magoli 121, Jose Mourinho msimu wa 2011/2012 alimaliza La Liga akiwa na mabao 121, hadi sasa Barcelona wana mabao 70 na itawabidi kufunga mabao 51 katika mechi zao 11 zilizobaki ili kuifikia rekodi ya Mourinho. Zamora award, hii ni tuzo ya kipa aliyefungwa mabao machache, Francisco Liano mlinda lango wa zamani wa klabu ya Sporting Gijon anashikilia rekodi ya kufungwa mabao machache zaidi La Liga, mabao 18 (1993/1994). Hadi sasa mlinda lango wa Atletico Madrid Jan Oblak ameruhusu mabao 12 katika lango lake huku golikipa wa Barcelona Marc Andre Stegen akiwa ameruhusu mabao 13 hadi sasa, na anasubiriwa kati ya hawa nani atavunja rekodi ya Liano. Real Sociedad record, Barcelona hawajapoteza katika michezo 32 ya La Liga na wamevunja rekodi ya Pep G...