Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tetesi za soka Ulaya Jumanne 16 Januari 2018

Arsenal wako kwenye mazungumzo kumsani mchezaji wa Borussia Dortmund na Gabon Pierre-Emerick Aubameyang kuchukua mahala pake Alexis Sanchez. (Mirror)

Arsenal wako mbioni na pauni milioni 53 kumpata Aubameyang 28. (Mail)
Na Jose Mourinho anasema kuwa hana ukakika kuwa atamleta Sanchez huko Manchester United. (Mirror)

Chelsea pia wamejiunga katika mbio za kumpata Sanchez lakini United wana uhakika kuwa kumpeana Henrikh Mkhitaryan, 28, kama sehemu ya makubaliano inawaweka katika nafasi nzuri. (Telegraph)

Mshambuliaji wa Real Madrid na Ureno Cristiano Ronaldo, 32, anataka kurudi Manchester United. (As.com - in Spanish)

Kiungo wa kati Emre Can, 24, anasema kuwa hajasaini makubaliano ya kujiunga na Juventus msimu huu na bado anazungumza na Liverpool kuhusu kuendelea kubaki huko Anfield. (Times - subscription required)

Swansea City wamefanya mazungumzo na Atletico Madrid kuhusu makubaliano ya kuwaleta mshambuliaji wa raia wa Ufaransa Kevin Gameiro 30, na mBrazil Nicolas Gaitan, 29, huko south Wales Januari hii. (Wales Online)

Everton wanajaribu kukamilisha makubaliano ya pauni milioni 20 kwa wing'a wa Arsenal na England Theo Walcott 28, wiki hii. (Mirror)

Bournemouth nao wamewajulisha Arsenal kuhusu kumchukua Walcott kwa mkopo kwa msimu wote. (Sun)

Sevilla wana uhakika wa kumpata kwa mkopo mshambuliaji wa Chelsea Michy Batshuayi, 24. (ESPN)

Meneja wa Wales Ryan Giggs anatathmini hatua ya kumfanya mchezaji mwenza katika Manchester United Paul Scholes kuwa mmoja wa kikosi chake. (Mail)

Mtaalamu wa masuala ya kandanda mfaransa Julien Lauren ana uhakika kuwa mshambulia wa PSG mBrazil Neymar 25, na mchezaji aliye kwenyr mkopo raia wa Ufaransa Kylian Mbappe, 19, wakati mmoja watakuwa wachezaji wa Real Madrid. (BBC Radio 5 live)

West Brom wanatoa ofa ya pauni milioni 12 kwa kiungo wa kati wa Fulham Tom Cairney, 26. (Sun)

Birmingham City wanataka kumsani beki wa Feyenoord Miquel Nelom, 27. (Mail)

Arsenal wako makini kumsaini kiungo wa kati wa Manchester United Henrikh Mkhitaryan 28, kama sehemu ya makubaliano ambayo yatamleta mshambuliaji raia wa Chile Alexis Sanchez, 29, huko Old Trafford. (Guardian)

Manchester City wamejitoa katika makubaliano ya kumsaini Sanchez na pesa zilizoitishwa na ajenti wake. (Goal.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Nitapindua dunia juu chini ili kubaki kama meneja wa Arsenal

Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake. Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal Kazi yake katika timu hiyo iliwekwa utatani wakati alipokataa kudhibitsha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror) Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)

Robert Lewandowski mfungaji bora Bundesliga 2017/2018

Robert Lewandowski amemaliza msimu wa 2017/18 wa Bundesliga akiwa mfungaji bora kwa mara ya 3 kwenye maisha yake ya soka. : • 30 games • 29 goals

Je Barcelona wataweza kuvunja rekodi hizi?

Hadi sasa miamba  ya Catalunya Fc Barcelona haijapoteza mchezo hata mmoja katika ligi kuu nchini Hispania na wanaonekana wanaweza kuweka rekodi ya kuwa timu pekee kumaliza La Liga bila kupoteza, lakini je na haya yafuatayo wataweza? Magoli 121, Jose Mourinho msimu wa 2011/2012 alimaliza La Liga akiwa na mabao 121, hadi sasa Barcelona wana mabao 70 na itawabidi kufunga mabao 51 katika mechi zao 11 zilizobaki ili kuifikia rekodi ya Mourinho. Zamora award, hii ni tuzo ya kipa aliyefungwa mabao machache, Francisco Liano mlinda lango wa zamani wa klabu ya Sporting Gijon anashikilia rekodi ya kufungwa mabao machache zaidi La Liga, mabao 18 (1993/1994). Hadi sasa mlinda lango wa Atletico Madrid Jan Oblak ameruhusu mabao 12 katika lango lake huku golikipa wa Barcelona Marc Andre Stegen akiwa ameruhusu mabao 13 hadi sasa, na anasubiriwa kati ya hawa nani atavunja rekodi ya Liano. Real Sociedad record, Barcelona hawajapoteza katika michezo 32 ya La Liga na wamevunja rekodi ya Pep G...