Chelsea wamezungumza na West Ham kuhusu kumsaini mshambuliaji wa miaka 29 Andy Carroll kwa mkataba wa kudumu. (Telegraph)
West Ham wanataka kuskiliza ofa ya pauni milioni 20 kwa Carroll. (Sky Sports)
Kiungo wa kati raia wa Armenia, Henrikh Mkhitaryan, 28, anasema anataka nyongeza ya mshahara kuweza kuhama Manchester United kwenda Arsenal. (Mirror)
Kiungo wa kati wa Arsenal na England Jack Wilshere, 26, ambaye mkataba wake unakamilika msimu huu ni lazima afanyiwe uchunguzi wa kiafya na kukubali mshahara wake kupunguzwa kwa asilimia 20 kuweza kupata mkataba mpya. (Sun)
Barcelona wamekataa ofa ya pauni milioni 22.2 kutoka Inter Milan kwa raia wa Brazil mwenye umri wa miaka 24 Rafinha kwa sababu wanataka pauni milioni 35.5.
Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger ana wasi wasi kuhusu kumsaini mshambuliaji mwenye hasira wa Borussia Dortmund Pierre-Emerick Aubameyang. (Star)
Tottenham ni kati ya vilabu vinavyommzea mate mchezaji wa hadhi juu wa Norwich James Maddison, 21. (London Evening Standard)
Kiungo wa kati wa Liverpool raia wa Serbia Marko Grujic, 21, analengwa kwa mkopo na Middlesbrough na Cardiff City. (ESPN)
Maoni
Chapisha Maoni