Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tetesi za soka Ulaya Jumatano 17 Januari 2018

Chelsea wamezungumza na West Ham kuhusu kumsaini mshambuliaji wa miaka 29 Andy Carroll kwa mkataba wa kudumu. (Telegraph)

West Ham wanataka kuskiliza ofa ya pauni milioni 20 kwa Carroll. (Sky Sports)

Kiungo wa kati raia wa Armenia, Henrikh Mkhitaryan, 28, anasema anataka nyongeza ya mshahara kuweza kuhama Manchester United kwenda Arsenal. (Mirror)

Kiungo wa kati wa Arsenal na England Jack Wilshere, 26, ambaye mkataba wake unakamilika msimu huu ni lazima afanyiwe uchunguzi wa kiafya na kukubali mshahara wake kupunguzwa kwa asilimia 20 kuweza kupata mkataba mpya. (Sun)

Barcelona wamekataa ofa ya pauni milioni 22.2 kutoka Inter Milan kwa raia wa Brazil mwenye umri wa miaka 24 Rafinha kwa sababu wanataka pauni milioni 35.5.

Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger ana wasi wasi kuhusu kumsaini mshambuliaji mwenye hasira wa Borussia Dortmund Pierre-Emerick Aubameyang. (Star)

Tottenham ni kati ya vilabu vinavyommzea mate mchezaji wa hadhi juu wa Norwich James Maddison, 21. (London Evening Standard)

Kiungo wa kati wa Liverpool raia wa Serbia Marko Grujic, 21, analengwa kwa mkopo na Middlesbrough na Cardiff City. (ESPN)

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Nitapindua dunia juu chini ili kubaki kama meneja wa Arsenal

Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake. Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal Kazi yake katika timu hiyo iliwekwa utatani wakati alipokataa kudhibitsha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror) Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)

Robert Lewandowski mfungaji bora Bundesliga 2017/2018

Robert Lewandowski amemaliza msimu wa 2017/18 wa Bundesliga akiwa mfungaji bora kwa mara ya 3 kwenye maisha yake ya soka. : • 30 games • 29 goals

Je Barcelona wataweza kuvunja rekodi hizi?

Hadi sasa miamba  ya Catalunya Fc Barcelona haijapoteza mchezo hata mmoja katika ligi kuu nchini Hispania na wanaonekana wanaweza kuweka rekodi ya kuwa timu pekee kumaliza La Liga bila kupoteza, lakini je na haya yafuatayo wataweza? Magoli 121, Jose Mourinho msimu wa 2011/2012 alimaliza La Liga akiwa na mabao 121, hadi sasa Barcelona wana mabao 70 na itawabidi kufunga mabao 51 katika mechi zao 11 zilizobaki ili kuifikia rekodi ya Mourinho. Zamora award, hii ni tuzo ya kipa aliyefungwa mabao machache, Francisco Liano mlinda lango wa zamani wa klabu ya Sporting Gijon anashikilia rekodi ya kufungwa mabao machache zaidi La Liga, mabao 18 (1993/1994). Hadi sasa mlinda lango wa Atletico Madrid Jan Oblak ameruhusu mabao 12 katika lango lake huku golikipa wa Barcelona Marc Andre Stegen akiwa ameruhusu mabao 13 hadi sasa, na anasubiriwa kati ya hawa nani atavunja rekodi ya Liano. Real Sociedad record, Barcelona hawajapoteza katika michezo 32 ya La Liga na wamevunja rekodi ya Pep G...