Sergio Aguero ametoa dondoo kuwa anaweza kuondoka Manchester City mwishoni mwa msimu huu.
Goal iliripoti mwezi Desemba kuwa Mwargentina huyo hana furaha katika klabu hiyo msimu huu baada ya kuachwa benchi mara nyingi na Pep Guardiola.
Na ingawa hataki kuondoka, amekiri kuwa klabu ndiyo yenye tamko la mwisho kwenye mustakabali wake.
Philippe Coutinho ameendelea kusisitiza kuwa anataka kuihama Liverpool ili ajiunge na Barcelona Goal imabaini.
Real Madrid wanataka kuvunja mkataba wa Kepa Arrizabalaga ili kuipata saini ya mlinda mlango huyo wa Athletic Club, kwa mujibu wa Marca .
Athletic hata hivyo hawana mpango wa kumuuza kipa huyo wa kimataifa wa Hispania, lakini Mabingwa hao wa Ulaya wanataka kutumia nguvu yao ya mshiko kumpata.
Real Madrid wapo tayari kumuuza Toni Kroos kwa Manchester United ikiwa ni sehemu ya jitihada zao kupata fedha ya kumsajili Neymar kutoka PSG kwa mujibu wa The Express .
West Ham wapo tayari kutoa kitita cha £15 milioni kumsajili Joe Allen kutoka Stoke City, kwa mujibu wa The Daily Mail .
David Moyes anataka kuimarisha safu yake ya kiungo majira ya baridi lakini Stoke City bado hawajawa tayari kumuuza Allen.
Maoni
Chapisha Maoni