Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tetesi za soka Ulaya Jumatatu 8 Januari 2018

Mshambuliaji wa Ufaransa Antoine Griezmann, 26, ataitisha pauni 400,000 kwa wiki kuzuia ofa ya Chelsea ili kujiunga na Manchester United. (Sun)

Chelsea wanamtaka mshambuliaji wa Borussia Monchengladbach na Ubelgiji Thorgan Hazard, 24, kujiunga na ndugu zake Eden, 27, na Kylian, 22, huko Stamford Bridge. (Bild - in German)

Liverpool wanamtaka mshambuliaji wa Monaco na Ufaransa Thomas Lemar, 22, kuchukua mahala pake Philippe Coutinho - na wanataka kufanya hilo wiki hii. (Mirror)

Manchester United na Chelsea zimemuulizia mshambuliaji wa Porto Mousa Marega, 26. (Metro)

Real Madrid walikuwa na nia ya kutoa ofa ya pauni milioni 177 kwa Coutinho kabla ya kukubali kujiunga na Barcelona kwa pauni milioni 142. (Mundo Deportivo - in Spanish)

Coutinho atafanyiwa uchunguzi wa kiafya leo Jumatatu na kutangazwa rasmi kama mchezaji wa Barcelona lakini kuanza kwake kucheza kunaweza kucheleweshwa kutokana na jeraha.

Nyota wa Barcelona Lionel Messi ametaka Philippe Coutinho kuwepo katika kikosi cha kwanza badala ya Ousmane Dembele. (Diario Gol)

Liverpool watajaribu kumleta kiungo wa kati wa RB Leipzig na Guinea Naby Keita Anfield na wana nia ya kulipa zaidi kumpata mchezaji huyo wa miaka 22 mwezi Januari. (Telegraph)

Wing'a mbrazil Lucas Moura, 25, anataka kuondoka Paris St-Germain kujiunga na Manchester United mwezi huu. (Telefoot via Express)

Real Madrid inapanga kuwasajili Eden Hazard, 27 na kipa Thibault Courtois, 25, kutoka Chelsea ifikapo mwisho wa msimu. Lakini watasubiri kuona hatma ya Harry Kane wa Tottenham

Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger anasema klabu yake haiko tayari kuongeza wachezaji zaidi Januari baada ya kumnunua kijana kutoka Ugiriki wa umri wa miaka 20, Konstantinos Mavropanos. (Sun)

Bournemouth wanatarajiwa kumsaini mfungaji bora zaidi wa Colchester United, Sammie Szmodics, 22, kwa gharama ya pauni milioni moja.

Kiungo wa kati wa Shakhtar Donetsk na Brazil Fred, 24, anasema anasubiri simu kutoka kwa meneja wa Manchester City Pep Guardiola. (GloboEsporte, kupitia Manchester Evening News)

NewCastle wana matumaini ya kumaliza kumsaini wing'a wa Chelsea mbrazil Kenedy, 21. (Newcastle Chronicle)
Leicester City wakaribia kumsaini mchezaji wake wa kwanza mwezi Januari - mshambuliajo wa Mali Fousseni Diabate.

The Foxes wamekubalia pauni milioni 1.7 kwa mchezaji huyo wa miaka 22 ambaye anacheza ligi ya pili ya Ufaransa Gazelec Ajaccio. (Leicester Mercury)

Leeds United wamemurodhesha beki wa Brugge ya Ubelgiji Laurens de Bock, 25, kuwa lengo lake kuu. (Leeds Live)

Mwanariadha nguli Usain Bolt, 31, amesema atafanya majaribio na Borussia Dortmund mwezi Machi, lakini anatamani sana kuichezea Manchester United. (Express)

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Nitapindua dunia juu chini ili kubaki kama meneja wa Arsenal

Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake. Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal Kazi yake katika timu hiyo iliwekwa utatani wakati alipokataa kudhibitsha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror) Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)

Robert Lewandowski mfungaji bora Bundesliga 2017/2018

Robert Lewandowski amemaliza msimu wa 2017/18 wa Bundesliga akiwa mfungaji bora kwa mara ya 3 kwenye maisha yake ya soka. : • 30 games • 29 goals

Je Barcelona wataweza kuvunja rekodi hizi?

Hadi sasa miamba  ya Catalunya Fc Barcelona haijapoteza mchezo hata mmoja katika ligi kuu nchini Hispania na wanaonekana wanaweza kuweka rekodi ya kuwa timu pekee kumaliza La Liga bila kupoteza, lakini je na haya yafuatayo wataweza? Magoli 121, Jose Mourinho msimu wa 2011/2012 alimaliza La Liga akiwa na mabao 121, hadi sasa Barcelona wana mabao 70 na itawabidi kufunga mabao 51 katika mechi zao 11 zilizobaki ili kuifikia rekodi ya Mourinho. Zamora award, hii ni tuzo ya kipa aliyefungwa mabao machache, Francisco Liano mlinda lango wa zamani wa klabu ya Sporting Gijon anashikilia rekodi ya kufungwa mabao machache zaidi La Liga, mabao 18 (1993/1994). Hadi sasa mlinda lango wa Atletico Madrid Jan Oblak ameruhusu mabao 12 katika lango lake huku golikipa wa Barcelona Marc Andre Stegen akiwa ameruhusu mabao 13 hadi sasa, na anasubiriwa kati ya hawa nani atavunja rekodi ya Liano. Real Sociedad record, Barcelona hawajapoteza katika michezo 32 ya La Liga na wamevunja rekodi ya Pep G...