Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Wenger na Pochettino wazozana

Kocha wa Arsenal wiki hii alitoa kauli ambayo imepokelewa vibaya na mashabiki wa Tottenham, wiki hii nzima mashabiki wa Tottenham mitandaoni wamekuwa wakimuandama Wenger.

Wakati Wenger akiongea na waandishi wa habari alisema anashangazwa na jinsi waandishi wanavyoongea kuhusu Arsenal kukosa makombe na huku kuna vilabu kama Tottenham na Liverpool nao wako hivyo hivyo.

Kocha wa Tottenham ameisikia kauli ya Wenger na kusema kwamba badala ya Wenger kujihusisha na kufuatilia mambo ya Tottenham inambidi awaze yeye kwanza kuhusu uwezo wao uwanjani.

Pochettino amesisitiza kwamba anamuheshimu sana Arsene Wenger na asingependa kupoteza heshima yake kwa kumuongelea vibaya lakini kwa sasa anaona ni vyema azungumzie masuala ya Arsenal zaidi.

Tottenham hawajachukua CL tangu mwaka 1984, hawajachukua EPL 1960/1961 na hawajachukua kombe la ligi tangu msimu wa 2007/2008 lakini Pochettino amesisitiza kwamba timu sio makombe tu ila hata wanavyokua ni jambo zuri.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Nitapindua dunia juu chini ili kubaki kama meneja wa Arsenal

Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake. Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal Kazi yake katika timu hiyo iliwekwa utatani wakati alipokataa kudhibitsha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror) Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)

Robert Lewandowski mfungaji bora Bundesliga 2017/2018

Robert Lewandowski amemaliza msimu wa 2017/18 wa Bundesliga akiwa mfungaji bora kwa mara ya 3 kwenye maisha yake ya soka. : • 30 games • 29 goals

Je Barcelona wataweza kuvunja rekodi hizi?

Hadi sasa miamba  ya Catalunya Fc Barcelona haijapoteza mchezo hata mmoja katika ligi kuu nchini Hispania na wanaonekana wanaweza kuweka rekodi ya kuwa timu pekee kumaliza La Liga bila kupoteza, lakini je na haya yafuatayo wataweza? Magoli 121, Jose Mourinho msimu wa 2011/2012 alimaliza La Liga akiwa na mabao 121, hadi sasa Barcelona wana mabao 70 na itawabidi kufunga mabao 51 katika mechi zao 11 zilizobaki ili kuifikia rekodi ya Mourinho. Zamora award, hii ni tuzo ya kipa aliyefungwa mabao machache, Francisco Liano mlinda lango wa zamani wa klabu ya Sporting Gijon anashikilia rekodi ya kufungwa mabao machache zaidi La Liga, mabao 18 (1993/1994). Hadi sasa mlinda lango wa Atletico Madrid Jan Oblak ameruhusu mabao 12 katika lango lake huku golikipa wa Barcelona Marc Andre Stegen akiwa ameruhusu mabao 13 hadi sasa, na anasubiriwa kati ya hawa nani atavunja rekodi ya Liano. Real Sociedad record, Barcelona hawajapoteza katika michezo 32 ya La Liga na wamevunja rekodi ya Pep G...