Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Zidane: "Hakuna Real Madrid bila Ronaldo"

Mkufunzi wa Real Madrid Zinedine Zidane anaamini kwamba mshambuliaji nyota Cristiano Ronaldo atasalia katika klabu hiyo na haoni sababu za yeye kuondoka katika klabu hiyo ya Uhispania.

Mshambuliaji huyo wa Ureno amefunga magoli tisa katika mechi sita za vilabu bingwa lakini amefunga bao nne katika mechi 14 za la Liga msimu huu.

Kulingana na ripoti , Ronaldo amekuwa na mgogoro wa kandarasi na klabu hiyo na amehusishwa na uhamisho wa kurudi Manchester United.

Lakini Zidane alisema: Mimi hupendelea kusema kitu hicho hicho kwamba sioni Real Madrid bila Cristiano Ronaldo.

Ronaldo mwenye umri wa miaka 32 yuko katika kandarasi hadi 2021 na alishinda taji lake la tano la Ballon d'Or mwezi uliopita, mbali na kufunga bao la pekee katika mechi ya fainali ya klabu bingwa duniani dhidi ya Gremio.

Licha ya kuonyesha mchezo mzuri katika mechi za vilabu bingwa, wako katika nafasi ya nne katika ligi ya La liga baada ya kushindwa nyumbani na Vilareal siku ya Jumamosi.

Tangu kujiunga na Real Madrid kutoka Man United ambapo alivunja rekodi ya £80m 2009, Ronaldo ameifungia timu yake mabao 422 katika mechi 418, lakini meshindwa kufunga katika mechi tatu za ligi.

Zidane alisema: Tunajua kilichojadiliwa , lakini kile Cristiano anachofaa kufanya ni kufikiria kucheza kama kawaida.

Ningependa kuzungumza kuhusu mchezo wake kwa sasa na kile anachoweza kuchangia katika timu akiwa uwanjani''.

''Cristiano ni mmoja wa klabu hii, ambapo yupo. Klabu, mashabiki na kila mtu anampenda. Upande wake wa mchezo ndio nilio na hamu nao. Sitaki kuzungumzia kandarasi yake na vitu kama hivyo''.

Baada ya kushinda mechi mbili kati ya saba za ligi, Real wako na pointi 19 nyuma ya viongozi Barcelona wakiwa na mechi ambayo hawajacheza.

Alipoulizwa kuhusu hatma yake ya siku za usoni , Zidane alisema: Sifikirii kuhusu hilo.Nafanya kazi kulingana na siku ilivyo na siwezi kubadilisha hilo.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Nitapindua dunia juu chini ili kubaki kama meneja wa Arsenal

Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake. Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal Kazi yake katika timu hiyo iliwekwa utatani wakati alipokataa kudhibitsha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror) Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)

Robert Lewandowski mfungaji bora Bundesliga 2017/2018

Robert Lewandowski amemaliza msimu wa 2017/18 wa Bundesliga akiwa mfungaji bora kwa mara ya 3 kwenye maisha yake ya soka. : • 30 games • 29 goals

Je Barcelona wataweza kuvunja rekodi hizi?

Hadi sasa miamba  ya Catalunya Fc Barcelona haijapoteza mchezo hata mmoja katika ligi kuu nchini Hispania na wanaonekana wanaweza kuweka rekodi ya kuwa timu pekee kumaliza La Liga bila kupoteza, lakini je na haya yafuatayo wataweza? Magoli 121, Jose Mourinho msimu wa 2011/2012 alimaliza La Liga akiwa na mabao 121, hadi sasa Barcelona wana mabao 70 na itawabidi kufunga mabao 51 katika mechi zao 11 zilizobaki ili kuifikia rekodi ya Mourinho. Zamora award, hii ni tuzo ya kipa aliyefungwa mabao machache, Francisco Liano mlinda lango wa zamani wa klabu ya Sporting Gijon anashikilia rekodi ya kufungwa mabao machache zaidi La Liga, mabao 18 (1993/1994). Hadi sasa mlinda lango wa Atletico Madrid Jan Oblak ameruhusu mabao 12 katika lango lake huku golikipa wa Barcelona Marc Andre Stegen akiwa ameruhusu mabao 13 hadi sasa, na anasubiriwa kati ya hawa nani atavunja rekodi ya Liano. Real Sociedad record, Barcelona hawajapoteza katika michezo 32 ya La Liga na wamevunja rekodi ya Pep G...