Liverpool imeshinda dhidi West Ham united 4 :1 leo Jumamosi Liverpool Wakiwa nyumbani katika uwanja wao wa Anfield.
Pande zote mbili zilipigiana mikwaju na mashuti makali katika wa dakika 15 za kwanza kabla ya Emre
Kuweza kuvunja ukimya kwa kichwa cha karibu na goli, akiifungia Liverpool goli la 100 msimu huu katika mashindano yote.
Kipindi cha pili kilikuwa cha neema na kwa vijana wa Liverpool hasa mshambuliaji wao hatari, Mmisri Mohamed Salah ambaye alifunga goli lake la 31 msimu huu.
Lakini pia wagonga nyundo hao wa London hawakumubali kubaki nyuma baada ya mchezaji wao wa akiba Michail Antonio kuwafungia goli baada ya kutoka benchi lakini Sadio Mane ndiye aliye pigia msumari wa mwisho katika ushindi huo mnono ulio iweka Liverpool katika nafasi ya pili.
Maoni
Chapisha Maoni