Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Ramos na rekodi ya ukorofi.

Wakati wakina Lionel Messi na Cristiano Ronaldo wanashindana kuweka rekodi za mabao na kufanya mambo mazuri katika soka, hali ni tofauti kwa mlinzi wa Real Madrid Sergio Ramos kwani anaweka rekodi za kihuni.
Rekodi zinaonesha Ramos ndio beki ambaye anacheza rafu mbaya zaidi katika ligi ya soka nchini Hispania La Liga suala ambalo limewalazimu waamuzi katika ligi hiyo kumpa kadi nyekundu 19.
Hakuna mchezaji yeyote tangu La Liga ianze ambaye amewahi kupewa kadi nyekundu kama ambavyo Sergio Ramos amepewa na ndio anashikilia rekodi ya kadi nyingi nyekundu katika michuano hiyo.
Ukiacha ufalme huo wa kadi alionao Ramos katika La Liga, sehemu pekee ambayo Ramos alikuwa amebakisha ni Champions League ambako huko Paul Scholes ndio alikuwa akishikilia rekodi ya kadi za njano akiwa na 36.
Lakini sasa Ramos amekaa juu ya Scholes kwani baada ya mchezo vs PSG sasa Ramos anakuwa na jumla ya kadi za njano 37 idadi ambayo hakuna mchezaji yeyote Champions League ambaye amewahi kupewa kadi nyingi za njano kama Ramos.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Nitapindua dunia juu chini ili kubaki kama meneja wa Arsenal

Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake. Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal Kazi yake katika timu hiyo iliwekwa utatani wakati alipokataa kudhibitsha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror) Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)

Robert Lewandowski mfungaji bora Bundesliga 2017/2018

Robert Lewandowski amemaliza msimu wa 2017/18 wa Bundesliga akiwa mfungaji bora kwa mara ya 3 kwenye maisha yake ya soka. : • 30 games • 29 goals

Je Barcelona wataweza kuvunja rekodi hizi?

Hadi sasa miamba  ya Catalunya Fc Barcelona haijapoteza mchezo hata mmoja katika ligi kuu nchini Hispania na wanaonekana wanaweza kuweka rekodi ya kuwa timu pekee kumaliza La Liga bila kupoteza, lakini je na haya yafuatayo wataweza? Magoli 121, Jose Mourinho msimu wa 2011/2012 alimaliza La Liga akiwa na mabao 121, hadi sasa Barcelona wana mabao 70 na itawabidi kufunga mabao 51 katika mechi zao 11 zilizobaki ili kuifikia rekodi ya Mourinho. Zamora award, hii ni tuzo ya kipa aliyefungwa mabao machache, Francisco Liano mlinda lango wa zamani wa klabu ya Sporting Gijon anashikilia rekodi ya kufungwa mabao machache zaidi La Liga, mabao 18 (1993/1994). Hadi sasa mlinda lango wa Atletico Madrid Jan Oblak ameruhusu mabao 12 katika lango lake huku golikipa wa Barcelona Marc Andre Stegen akiwa ameruhusu mabao 13 hadi sasa, na anasubiriwa kati ya hawa nani atavunja rekodi ya Liano. Real Sociedad record, Barcelona hawajapoteza katika michezo 32 ya La Liga na wamevunja rekodi ya Pep G...