Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tetesi za soka Ulaya na Alhamisi Machi 1 2017

West Ham iko tayari kumsiani mlinzi wa Ireland Kaskazini Jonny Evans, 30, kwa paundi milioni tatu kutoka kwa West Brom ikifika mwisho wa msimu. (Birmingham Mail)

Kiungo wa Arsenal na timu ya England, Jack Wilshere, 26 anasema atatoka kwenye klabu hiyo kati kati ya mwaka huu, wasipo mpatia mkataba bora zaidi. (Sun)

Manchester United kuachana na mipango ya kuupanua uwanja wa Old Trafford mwaka huu na kujikita zaidi katika kumuunga mkono Jose Mourinho katika kutafuta wachezaji.(Mail)

Winga wa Chelsea kutoka Brazil,Willian,29, anaweza iacha Stamford Bridge katikati ya mwaka na huenda akujiunga na timu ya AC Milan au Manchester United (Star)

Manchester United wameuongeza muda ya mikataba ya viungo Ashley Young, 32, na Daley Blind, 27, na ule wa mlinda mlango Sam Johnstone, 24

Mashetani hao wekundu wana waacha viungo Marouane Fellaini, 30, na Michael Carrick, 36, na mshambuliaji Zlatan Ibrahimovic ambao watakuwa huru kuondoka na kwa usajili huru majira ya joto.

Alan Pardew atafukuzwa kazi itakapotekea WestBrom watashindwa na Watford Jumamosi. (Mirror)

Nao Juventus wanatamani kumalizia kumsajili kiungo Emre Can, 24, ilikuzuia kuingia kwenye mndada wa kimataifa Ujerumani wakati wa majira ya joto. (La Gazzetta dello Sport)

Liverpool na Barcelona wamevutiwa na kiungo wa Lyon mwenye miaka 19, Houssem Aouar. Kijana huyo Mfaransa amecheza mara 17 kwenye Ligue ya kwanza. (Goal)

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Nitapindua dunia juu chini ili kubaki kama meneja wa Arsenal

Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake. Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal Kazi yake katika timu hiyo iliwekwa utatani wakati alipokataa kudhibitsha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror) Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)

Robert Lewandowski mfungaji bora Bundesliga 2017/2018

Robert Lewandowski amemaliza msimu wa 2017/18 wa Bundesliga akiwa mfungaji bora kwa mara ya 3 kwenye maisha yake ya soka. : • 30 games • 29 goals

Je Barcelona wataweza kuvunja rekodi hizi?

Hadi sasa miamba  ya Catalunya Fc Barcelona haijapoteza mchezo hata mmoja katika ligi kuu nchini Hispania na wanaonekana wanaweza kuweka rekodi ya kuwa timu pekee kumaliza La Liga bila kupoteza, lakini je na haya yafuatayo wataweza? Magoli 121, Jose Mourinho msimu wa 2011/2012 alimaliza La Liga akiwa na mabao 121, hadi sasa Barcelona wana mabao 70 na itawabidi kufunga mabao 51 katika mechi zao 11 zilizobaki ili kuifikia rekodi ya Mourinho. Zamora award, hii ni tuzo ya kipa aliyefungwa mabao machache, Francisco Liano mlinda lango wa zamani wa klabu ya Sporting Gijon anashikilia rekodi ya kufungwa mabao machache zaidi La Liga, mabao 18 (1993/1994). Hadi sasa mlinda lango wa Atletico Madrid Jan Oblak ameruhusu mabao 12 katika lango lake huku golikipa wa Barcelona Marc Andre Stegen akiwa ameruhusu mabao 13 hadi sasa, na anasubiriwa kati ya hawa nani atavunja rekodi ya Liano. Real Sociedad record, Barcelona hawajapoteza katika michezo 32 ya La Liga na wamevunja rekodi ya Pep G...