Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Arsenal na rekodi mbovu ugenini.

Pierre-Emerick Aubameyang anaweza kuwa mchezaji wa kwanza wa Araenal kufunga mabao katika mechi 5 mfululizo za Arsenal tangu Olivier Giroud afanye hivyo wakati yupo Arsenal mwaka 2015.

Tayari Arsenal wamepoteza michezo 4 mfululizo ugenini,mara ya mwisho wanapoteza mechi 5 mfululizo ugenini ilikuwa 1984/1985 na mwaka huo baada ya mechi hizo walizopoteza ugenini walipata ushindi wa kwanza katika uwanja ambao leo ndio wanakwenda wa St James Park.

Na kama hujui tu ni kwamba Arsenal hawajawahi kupoteza michezo 5 mfululizo ya ugenini katika calender ya mwaka mmoja tangu wafanye hivyo mwaka 1925, na kama leo watakubali kufungwa itakuwa mara yao ya kwanza ndani ya miaka 93.

Lakini Newcastle wenyewe wanaonekana nj wanyonge sana kwa Arsenal, katika michezo 10 iliyopita ya Newcastle mbele ya Arsenal wamekubali kupoteza michezo yotee mbele ya washika mtutu hao wa London.

Bao la Nolberto Solano mwaka 2005 ambalo liipa ushindi Newcastle mbele ya Arsenal, ndio ushindi wa mwisho kwa Newcastle mbele ya Arsenal na tangu hapo wamekuwa wakichezea kichapo tuu.

Lakini Arsenal huwa wanawafunga Newcastle bao moja tu, na Arsenal wameifunga Newcstle 1-0 kuliko timu yoyote EPL. Michezo 9/26 waliyowafunga Newcastle wamewafunga kwa bao moja tu ikiwemo michezo yao mitati ya mwisho.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Nitapindua dunia juu chini ili kubaki kama meneja wa Arsenal

Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake. Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal Kazi yake katika timu hiyo iliwekwa utatani wakati alipokataa kudhibitsha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror) Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)

Robert Lewandowski mfungaji bora Bundesliga 2017/2018

Robert Lewandowski amemaliza msimu wa 2017/18 wa Bundesliga akiwa mfungaji bora kwa mara ya 3 kwenye maisha yake ya soka. : • 30 games • 29 goals

Je Barcelona wataweza kuvunja rekodi hizi?

Hadi sasa miamba  ya Catalunya Fc Barcelona haijapoteza mchezo hata mmoja katika ligi kuu nchini Hispania na wanaonekana wanaweza kuweka rekodi ya kuwa timu pekee kumaliza La Liga bila kupoteza, lakini je na haya yafuatayo wataweza? Magoli 121, Jose Mourinho msimu wa 2011/2012 alimaliza La Liga akiwa na mabao 121, hadi sasa Barcelona wana mabao 70 na itawabidi kufunga mabao 51 katika mechi zao 11 zilizobaki ili kuifikia rekodi ya Mourinho. Zamora award, hii ni tuzo ya kipa aliyefungwa mabao machache, Francisco Liano mlinda lango wa zamani wa klabu ya Sporting Gijon anashikilia rekodi ya kufungwa mabao machache zaidi La Liga, mabao 18 (1993/1994). Hadi sasa mlinda lango wa Atletico Madrid Jan Oblak ameruhusu mabao 12 katika lango lake huku golikipa wa Barcelona Marc Andre Stegen akiwa ameruhusu mabao 13 hadi sasa, na anasubiriwa kati ya hawa nani atavunja rekodi ya Liano. Real Sociedad record, Barcelona hawajapoteza katika michezo 32 ya La Liga na wamevunja rekodi ya Pep G...