Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Liverpool watinga fainali ligi ya mabingwa ulaya

Pamoja na kipigo cha mabao 4-2 kutoka kwa As Roma, lakini Liverpool wamefanikiwa kufudhu kwenda fainali ya michuano ya Champions League kwa aggregate ya mabao 6-7, na hii ikiwa ni fainali yao ya 8 wanakwenda.

Roberto Firminho alitoa assist iliyozaa bao la kwanza la Liverpool lililofungwa na Sadio Mane, assist ya Firminho inamfanya kuwa mchezaji wa kwanza katika miaka 10 ya mwisho ya CL kuwahi kuwa na walau mabao 7 na assist 7 katika msimu mmoja wa CL.

Dakika ya 15 ya mchezo, As Roma walipata bao baada ya James Milner kujifunga. Hili linakuwa bao la kwanza kwa Liverpool kujifunga tangu Johne Arne Riise ajifunge katika mchezo wa nusu fainali vs Chelsea msimu wa 2007/2008.

Dakika ya 25 Liverpool walipata tena bao la kuongoza kupitia kwa Gerginio Wijnaldum, na hili likiwa bao la 19 kwa Wijnaldum kuwahi kuzifungia timu za Uingereza, 11 akiwafungia Newcastle na 8 akiwafungia Liverpool.

Bao la Mane limeufanya utatu wa Liverpool kufikisha jumla ya mabao 29 katika Champions League msimu huu, sasa Mane, Salah na Firmino wanakuwa wamefunga mabao mengi kuliko Bale, Benzema na Cr7 walivyofunga msimu wa 2013/2014 (28).

Bao la leo la Edin Dzeko linamfanya kufunga mabao 5 katika mechi 5 mfululizo za CL na sasa anakuwa mchezaji wa kwanza wa As Roma kuwahi kufunga mabao 5 katika michezo 5 mfululizo ya klabu hiyo katika Champions League.

Lakini pia bao la Edin Dzeko linamfanya kuifikia rekodi ya Samuel Etoo ya mchezaji wa klabu toka Italia kuwahi kufunga mabao 8 katika Champions League, rekodi aliyoweka mwaka 2010/2011, Radja Nainggolan alifunga mabao mengine mawili kwa As Roma.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Nitapindua dunia juu chini ili kubaki kama meneja wa Arsenal

Uongozi wa timu ya Arsenal wamemgeukia meneja wao, Arsene Wenger na kuanza kuorodhesha majina mbadala kuchukua nafasi yake. Wenger anasema "atapindua dunia chini juu" ilikubaki kama meneja wa Arsenal Kazi yake katika timu hiyo iliwekwa utatani wakati alipokataa kudhibitsha kama ataendelea na mkataba wake unaoisha 2019. (Mirror) Aliyekuwa rais wa timu ya Barcelona Joan Laporta, amesema anawahimiza Arsenal kumfikiria Thierry Henry kama mbadala wa Wenger.(Telegraph)

Robert Lewandowski mfungaji bora Bundesliga 2017/2018

Robert Lewandowski amemaliza msimu wa 2017/18 wa Bundesliga akiwa mfungaji bora kwa mara ya 3 kwenye maisha yake ya soka. : • 30 games • 29 goals

Je Barcelona wataweza kuvunja rekodi hizi?

Hadi sasa miamba  ya Catalunya Fc Barcelona haijapoteza mchezo hata mmoja katika ligi kuu nchini Hispania na wanaonekana wanaweza kuweka rekodi ya kuwa timu pekee kumaliza La Liga bila kupoteza, lakini je na haya yafuatayo wataweza? Magoli 121, Jose Mourinho msimu wa 2011/2012 alimaliza La Liga akiwa na mabao 121, hadi sasa Barcelona wana mabao 70 na itawabidi kufunga mabao 51 katika mechi zao 11 zilizobaki ili kuifikia rekodi ya Mourinho. Zamora award, hii ni tuzo ya kipa aliyefungwa mabao machache, Francisco Liano mlinda lango wa zamani wa klabu ya Sporting Gijon anashikilia rekodi ya kufungwa mabao machache zaidi La Liga, mabao 18 (1993/1994). Hadi sasa mlinda lango wa Atletico Madrid Jan Oblak ameruhusu mabao 12 katika lango lake huku golikipa wa Barcelona Marc Andre Stegen akiwa ameruhusu mabao 13 hadi sasa, na anasubiriwa kati ya hawa nani atavunja rekodi ya Liano. Real Sociedad record, Barcelona hawajapoteza katika michezo 32 ya La Liga na wamevunja rekodi ya Pep G...