Zikiwa zimebaki mechi mbili msimu wa 2017/18 wa La Liga kumalizika, Real Madrid wana pointi 72 na endapo watashinda mechi zao zote wataishia kupata pointi 78 tu.
Msimu wa mwisho Real Madrid kupata pointi chache zaidi kwenye La Liga, ulikuwa msimu wa 2008/09 - ambapo Los Blancos wakiwa chini ya Juande Ramos, hawakushinda taji lolote, wakiwaangalia Barcelona chini ya Pep Guardiola wakishinda mataji matatu na kuwafunga Madrid 6-2 nyumbani kwao Bernabeu. :
Msimu huu mambo yanaweza kuwa tofauti, Madrid wapo kwenye fainali ya ulaya na endapo watashinda watakuwa wamefanikiwa kimataifa lakini watakuwa wamefeli nyumbani tena - mpaka hivi sasa wapo nyuma kwa pointi 18 nyuma ya Wakatalunya ambao tayari wameshabeba ubingwa.
Leo usiku Madrid atakuwa akiumana na Celta Vigo
Maoni
Chapisha Maoni