Shirikisho la soka Soka nchini Uingereza (FA) limemshtaki meneja wa Manchester City juu ya kuvaa kwake Ribbon ya njano katika miezi ya hivi karibuni.
Guardiola alivaa Ribbon hio ili kuonyesha msaada wake kwa wanaharakati na wafungwa kisiasa ambao walijitangazia uhuru wa Katalani.
Uhalali wa Ribbon katika soka ya Kiingereza haukuwa na shaka, kama Jose Mourinho aliuliza katika mkutano wa waandishi wa habari mnamo Desemba kama ujumbe huo wa kisiasa unapaswa kuruhusiwa.
Kwa mujibu wa sheria 4.5. ya Sheria ya Mpira wa Kimataifa wa Chama cha Soka (IFAB), wachezaji na makocha haruhusiwi kuvaa vifaa na "slogans yoyote ya kisiasa, kidini au binafsi".
Na FA imeamua kutambua Ribbon ya Guardiola kama uvunjaji wa sheria na itachukua hatua za kumuadhibu kocha wa Manchester City .
"Pep Guardiola ameshtakiwa kwa kuvaa ujumbe wa kisiasa, hasa Ribbon ya njano, kwa ukiukaji wa kanuni za FA na matangazo," taarifa kutoka FA inasema.
KhaKhaaaaaaaaaaaaaaa
JibuFuta